Gazeti lingine lafungiwa na serikali kwa siku 90...Soma habari kamili na Matukio360...#share

SERIKALI imelifungia Gazeti la Tanzania Daima kwa siku 90, kwa kile kinachodaiwa kuchapisha makala na habari zinazokiuka misingi na maadili ya uandishi wa habari.
Gazeti la Tanzania Daima lililofungiwa kwa siku 90 na serikali.

Hayo yamebainishwa leo katika taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dk. Hassan Abbas akieleza sababu za serikali kulifungia gazeti hilo.

“Hatua hii inafuatia mfululizo wa gazeti hili kucapsha habari na Makala zenye uchuchezi, lakini vile vile zinazokiuka misingi na maadili ya uandishi wa habari, lakini vile vile na sharia za nchi,” amesema Dk. Abbas.

Kufungiwa kwa Gazeti hilo kuna kuja baada ya serikali kuwa imekwisha yafungia magazeti mengine ya Mwanahalisi, Mawio na Raia Mwema kutokana na kudaia kuandika habari zinadaiwa ni za kichochezi.

Taarifa kamili ya serikali





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search