George Bush aomba msamaha...soma habari kamili na Matukio360...#share

RAIS mstaafu wa Marekani George Bush ameomba msamaha kwa dhihaka aliyosababisha baada ya muigizaji, Heather Lind kumtuhumu kuwa alimnyanyasa kijinsia.

Heather Lind mwanamke anayedai kunyanyaswa kijinsia na rais mstaafu wa Marekani, George Bush
Heather Lind amesema rais huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 93 alimshika kutoka nyuma akiwa katika kiti chake cha magurudumu na kutamka ''mzaha mchafu'' wakati wakijiandaa kupiga picha.

Bi Lind alitoa madai hayo katika mtandao wa Instagram katika chapisho ambalo limefutwa.

Hata hivyo msemaji wa Bush amesema  tukio hilo  lililotokea mwaka 2014 lilikuwa jaribio la ucheshi.

''Rais Bush alikuwa hawezi chini ya hali yoyote ile na kwa makusudi kumsababishia mtu dhihaka na ameomba msamaha iwapo kitendo chake cha kuzua ucheshi kilimkosea bi Lind'', taarifa iliosambazwa kwa vyombo vya habari inasema.


Mitandao yote ilihifadhi chapisho hilo la Lind kabla ya kufutwa. Bush alihudumu katika kipindi cha miaka mitano kutoka 1989 hadi 1993 na ni babake George W Bush ambaye alihudumu mihula miwili kati ya 2001 hadi 2009. Mzee huyo anaugua ugonjwa wa kutetemeka.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search