Watendaji kata, vijiji wachapwa viboko, Serikali kufuta ajira zao...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
WAKULIMA na wafugaji waliopo katika eneo la hifadhi na misitu asili wilayani Chunya mkoani Mbeya wanawachapa viboko watendaji kata na vijiji.


Mkuu wa wilaya ya Chunya mkoani Mbeya, Rehema Madusa

Kauli hiyo imetolewa leo na mtendaji wa kata ya Mafyeko wilayani humo, Lucas Ongara kwenye kikao kazi cha kuweka mikakati ya kuboresha  sekta ya kilimo mwaka 2017/18 kilichohudhuriwa na mkuu wa wilaya ya Chunya, Rehema Madusa.

Amesema wanakabiliana na changamoto  hiyo  kutokana na makazi ya wakulima na wafugaji kuwepo  katikati ya mapori ya hifadhi na mara nyingi wanapofuatilia wanatekwa na kucharazwa viboko.

"Tatizo sio kamba tunashindwa kuwaondoa  wavamizi maeneo wanayoishi ni hatarishi na wana roho za kikatiri na wanauongozi wao ambao sio wa serikali na wana maamuzi ya kufanya lolote sasa na sisi ni binadamu tunahofia uhai wetu,"amesema.

Ametoa kauli hiyo kufuatia mkuu wa wilaya ya Chunya kutoa  siku sita na kuwa atasitisha ajira  za watendaji ngazi za kata na vijiji watakaoshindwa kuwaondoa  wakulima na wafugaji waliovamia  maeneo ya hifadhi na misitu ya asili.
  
“Kuna kasumba ya watendaji na wenyeviti wa vijiji
kuuza maeneo  katika  hifadhi jambo linalosababisha serikali kuingia gharama ya kuwaondoa wakulima na wafugaji kwa kuteketeza makazi yao.

"Siwezi kuvumilia au kukaa na watu wasioitakia mema serikali kwa kutanguliza maslai ya fedha mbele, Chunya imeharibiwa katika maeneo ya hifadhi. Natoa siku sita  muwaondoe wote waliovamia maeneo ya hifadhi. La Sivyo nitasitisha ajira za watendaji wa kata na vijiji.”  amesema

Pia amewaagiza watendaji kuhakiki vijiji hewa visivyokuwa katika mpango wa matumizi bora ya ardhi na idadi ya wakulima ili kufanya tathimini ya mahitaji  hususan upatikanaji wa pembejeo za kilimo na kuwaingiza katika vijiji vinavyotambuliwa kisheria .

Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Chunya, Ester Mwakalile ameahidi  kusimamia utekelezaji wa maagizo hayo  na kuonya watendaji
na wenyeviti wa vijiji kuacha kufanya kazi kwa mazoea na kujilimbikizia mali kupitia migongo ya wakulima na wafugaji .


Mkulima wa kijiji cha Sangambi, Athanas Mabul amesema hawapingani na serikali ila viongozi wa ngazi za kata na vijiji wanawachangisha fedha kwa madai zinapelekwa serikali hali inayopelekea kwenda katika maeneo ya hifadhi.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search