Mbeya kuhakiki vyeti vya maafisa ugani...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Mwandishi wetu
MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amemwagiza kaimu katibu Tawala Mkoa, Costantine Mushi kufanya uhakiki wa vyeti kwa  maofisa ugani kuanzia ngazi ya kata,kijiji  na halmashauri  ili kubaini wanaostahili kuwepo katika ajira serikalini

Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla
Makalla ametoa agizo hilo kwenye kikao maalum cha kazi kilichohusisha wakuu wa wilaya, wakurugenzi, wakuu wa idara, maofisa kilimo na mifugo wa  halmashauri wakati wa kikao cha kazi cha kujadili
mikakati ya kuboresha sekta ya kilimo mwaka 2017/18.

Amesema  kuna kasumba ya maofisa ugani kutojua majukumu yao sehemu za kazi hali inayosababisha kutoa takwimu za uongo  za uzalishaji  wa mazao ya chakula na biashara

"Nimebaini  wapo  maofisa ugani ambao hawana  sifa sasa katibu Tawala haraka anza  zoezi la uhakiki wa vyeti kabla ya msimu wa kilimo haujaanza. Lengo la Serikali ni kuwa na wataalam wanaowafikia wakulima vijijini na  si kukaa maofisini. "amesema.

Aidha ameonya maofisa kilimo na mifugo katika halmashauri zote kuacha kufanya kazi kwa mazoea na kushindwa kusimamia majukumu yao na kuwa
Ni bora serikal ibaki na watu wachache wanaotambua majukumu  yao na si kuwa na idadi kubwa ya watumishi wanaopata mishahara ya bure .

Naye Ofisa Kilimo Mkoa wa Mbeya, Enock Nyasebwa amesema  mkoa umeweka lengo la kuzalisha  tani 3.9 za mazao ya chakula na biashara mwaka 2017/18.

Pia kutoa elimu kwa maofisa ugani na wakulima ili
kufikia lengo walilokusudia la kuzalisha mazao yaliyo na tija katika kuelekea uchumi wa viwanda.

Akizungumza kwa niaba ya wakuu wa wilaya, mkuu wa wilaya ya Rungwe, Julius Chalya amesema  watatekeleza agizo la mkuu wa mkoa, kwa kuanza uhakiki ili kuiwezesha Serikali kupata wataalam watakayoifikisha Tanzania katika  uchumi wa viwanda.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search