Rais mstaafu Goodluck Jonathan aitwa mahakamani .Soma habari kamili na Matukio360..#share
JAJI wa Mahakama Kuu nchini Nigeria ameamuru rais wa zamani
wa nchi hiyo, Goodluck Jonathan apewe hati ya kuitwa mahakamani kuhusu kesi ya
rushwa inayomkabili msemaji wake wa zamani katika chama cha Peoples Democratic
Party (PDP).
Rais wa zamani wa Nigeria, Goodluck Jonathan
Hatua hiyo inatajwa kama ya kushangaza na ambayo itafuatiliwa kwa karibu kutokana na kwamba Jonathan amekuwa akitajwa katika matukio mengi ya kifisadi japokuwa hakuwahi kuitwa na kuhojiwa rasmi.
Msemaji wa zamani wa rais huyo, Olisa Metuh anakabiliwa na kesi anayoshtakiwa kwa kosa la kujipatia kwa njia za udanganyidui dola 1.1 milioni za Marakeni kutoka kwa Sambo Dasuki mshauri wa masuala ya usalama wa Jonathan.
Hatua hiyo inatajwa kama ya kushangaza na ambayo itafuatiliwa kwa karibu kutokana na kwamba Jonathan amekuwa akitajwa katika matukio mengi ya kifisadi japokuwa hakuwahi kuitwa na kuhojiwa rasmi.
Msemaji wa zamani wa rais huyo, Olisa Metuh anakabiliwa na kesi anayoshtakiwa kwa kosa la kujipatia kwa njia za udanganyidui dola 1.1 milioni za Marakeni kutoka kwa Sambo Dasuki mshauri wa masuala ya usalama wa Jonathan.
Katika utetezi wake, msemaji huyo ameng’ang’ania kwamba
alipokea fedha hizo kwa maelekezo yaliyotolewa na Jonathan ili kugharimia
kampeni za kutetea kiti chake mwaka 2015.
Jumatatu, mawakili wa Metuh walisema kwamba wanakusudia
kumwita rais huyo wa zamani kama shahidi.
Jaji wa Mahakama Kuu ya Shirikisho Abang Okon anayesikiliza
shauri hilo alisema itakuwa “sawa na ukiukwaji wa haki zake (Metuh) kwa
usikilizwaji wa haki ikiwa hatatia saini hati ya kuitwa mahakamani".
"Sina chaguo jingine zaidi ya kutia saini hati ya
mahakama ya kumlazimisha rais wa zamani Goodluck Jonathan kufika mahakamani
jana Oktoba 25, 2017 ili aweze kutoa ushahidi wake," amesema.
No comments:
Post a Comment