Mkurugenzi Chadema, Benson kufikishwa Mahakamani...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
MKURUGENZI wa Operesheni na Mafunzo wa chama cha Chadema, Kigaila Benson uenda kesho akafikishwa Mahakamani kwa madai ya kutoa lugha ya  uchochezi na  kashfa.


Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, SACP Lazaro Mambosasa 
Chanzo chetu kutoka Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, kimesema Benson alitakiwa kufikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Ijumaa iliyopita lakini ilishindikana.

‘NI uhakika kesho Jumatatu, Kigaila Benson atafikishwa katika mahakama ya kisutu kujibu mashtaka yanayomkabili. Ilitakiwa afikishwe Ijumaa iliyopita lakini kutokana na sababu kadhaa ikashindikana,’ kimesema chanzo chetu hicho

Hivi karibuni Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, SACP Lazaro Mambosasa alithibitisha kukamatwa kwa Mkurugenzi huyo kwa mahojiano kwa madai ya kutoa lugha ya kuikashfu serikali na watu wake.

Alisema "Tunaendelea kumshikilia na anaendelea kuhojiwa atakapokamilisha yale ambayo yanamuhusu tutaelekeza kesi mahakamani kama ushahidi utakuwepo wa kutosha,"amesema.


Mambosasa amesema endapo ushahidi utakuwa wa kuendelea na mashahidi wengine wataangalia kupata dhamana huko mbele kwani jeshi hilo halijakamilisha yale waliokusudia.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search