Zitto 'kuidadavua' serikali leo...soma habari kamili na Matukio360...#share
Na mwandishi wetu
CHAMA cha ACT
Wazalendo leo kinazindua kampeni zake rasmi za kugombea nafasi ya udiwani katika
kata 43 nchini.
Zitto Kabwe ambaye ni kiongozi mkuu wa ACT Wazalendo akiwa katika moja ya mikutano ya hadhara ya kampeni
Afisa habari wa ACT
Wazalendo, Abdallah Khamis ameiambia Matukio360 kuwa kiongozi mkuu wa ACT
Wazalendo, Zitto Kabwe atazindua kampeni hiyo leo jijini Dar es Salaam katika
kata ya Kijichi.
Pia viongozi wengine
wa kitaifa watakuwapo na kwamba mgombea wa udiwani wa kata hiyo wa ACT Wazalendo, Mkosamali Edga anayetarajia kupambana
na vyama vingine ikiwamo CCM na Ukawa, atatambulishwa rasmi
Uchaguzi huo mdogo wa
marudio wa udiwani utafanyika Novemba 26, 2017, utahusisha kata 43 nchini, Dar
es salaam ikihusisha kata ya Mbweni, Kijichi na Saranga
Akunukuliwa jana Zitto
ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma mjini amesema utafiti walioufanya unaonyesha
chama hicho kinaweza kuchukua kata za Kijichi na Saranga endapo vyama vingine
vya upinzani vitakiachia ACT Wazalendo.
Mkutano huo utafanyika
katika viwanja vya Centre Kijichi kuanzia majira ya saa tisa Alasir
No comments:
Post a Comment