Mshambuliaji wa Zamani Arsenal Ian Wright Ataja Mrithi wa Wenger..Soma Habari Kamili na Matukio360...#share


 MSHAMBULIAJI wa Zamani wa Klabu ya Arsenal ambaye kwa sasa ni Mchambuzi wa Kituo cha BBC Sport Ian Wright anaamini kuwa kocha wa Burnley  Sean Dyche ana ubora wa kuweza kuongoza vilabu vikubwa vya nchini Uingereza.
Image result for arsenal wenger
 Klabu ya Burnley kwa sasa katika msimamo wa ligi Kuu ya Uingereza (Premier League) wanashika nafasi ya sita baada ya kuifunga Evertoni nyumbani kwake mwishoni mwa wiki iliyopita. 

Baada ya kujiunga na Klabu ya Lancashire mwaka 2012, Dyche ameweza kuiongoza Burnley kwa misimu miwili kwa michezo ya kupanda ligi kuu na waliweza pia kushuka daraja misimu mitano iliyopita.

 "Nina amini yeye (Dyche) ni mtu fulani ambaye anahiaji kupiga hatua hatua fulani, katikamhatua nyingine,” Wright ameiambia BBC Radio 5 live.

"Ni kocha mwenye uzoefu katika Premier League. Ameshafanya kazi nzuri na timu ndogo na zimeweza kufanya vizuri,”. Ameongeza.
 
Arsene Wenger aliongeza mkataba wa miaka miwili mwezi wa Juni mwaka huu baada ya kuwepo kwa tetesi nyingi kuhusu kuendelea au kutoendelea kuifundisha klabu ya Arsenal.

Wright alipoulizwa kama  Dyche anafiti kuirithi mikoba ya Wenger  Arsenal, alijibu: "Ndiyo. Je ukweli ni kwamba watampa Sean Dyche kazi hiyo?

"Kwa kuheshimu namna alivyoitengeneza timu yake jinsi wanavyo ziuia, ni wazi yuko vizuri, lakini je atapewa kazi kama hiyo? Si fikiri kama atapewa.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search