Ndege yaanguka na kujeruhi 11...Soma habari kamili na Matukio360..#share

MAPEMA mchana wa leo ndege aina ya Cessna Grand Caravan ikiwa na abiria 11 na Rubani imeanguka ikiwa angani maeneo ya Mbuga ya Serengeti.

Katika ajali hiyo abiria wawili  na rubani ambao walipata majeraha makubwa, walisafirishwa kwenda Nairobi kwa ajili ya kupata huduma ya matibabu kwa msaada wa watu wa Coastal  huku waliobaki wakipata majeraha madogo madogo.

Kwa Mujibu wa Mkurugenzi, Julian Edmunds, ambaye alikuwemo katika ndege hiyo ambayo ilikuwa imetokea Nairobi nchini Kenya, ameeleza kuwa miongoni mwa majeruhi hakuna ambaye alipata majeraha yakutisha.


Inasemekana ajali hiyo imechangiwa na mvua ambayo ilifanya  rubani ashindwe kuona vizuri hivyo Wakati anajaribu kutua akajikuta ameshafika katikati ya uwanja hali iliyomfanya apitilize na kugonga miti na mawe. 




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search