UDART yasimamisha usafiri mabasi ya mwendo kasi...Soma habari kamili na Matukio360..#share

                    
KAMPUNI inayotoa huduma kwenye mradi wa mabasi yaendayo haraka UDART, imetangaza kusitisha huduma hiyo kuanzia mchana mchana wa leo.
Basi la usafiri wa haraka ya UDART

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa umma na Deus Bugaywa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, amesema sababu za kusitisha huduma hiyo ni kutokana na kufungwa kwa barabara ya Morogoro baada ya daraja la mto Msimbazi kujaa maji.

“Tunaujulisha umma kuwa huduma hiyo imesitishwa kwa muda kuanzia saa 7:30 mchana wa Alhamis Oktoba, 26, 2017, kutokana na kufungwa kwa Barabara ya Morogoro kwa sababu ya daraja la mto Msimbazi kujaa maji,” imesema taarifa hiyo.


Aidha imeeleza kuwa huduma itarejea mara baada ya hali kutengemaa, hivyo kutokana na hali hiyo kampuni imeomba radhi abiria kwa usumbufu uliojitokeza.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search