Ni Cristiano Ronaldo tena...soma habari na Matukio360...#share

CRISTIANO Ronaldo ameshinda taji la shirikisho la soka FIFA la mchezaji bora wa kiume wa mpira wa miguu mwaka 2017 ikiwa ni mara ya pili mfululizo.

Mchezaji soka,Christiano Ronaldo
Mchezaji huyo kutoka Ureno, amefunga mabao 44 katika mechi 48 alizoshiriki katika mwaka, kuiwakilisha nchi yake pamoja na timu anayoichezea ya Real Madrid aliochangia kufanikisha ushindi wake katika mataji ya ligi ya Uhispania La Liga na ligi ya mabingwa Ulaya - Champions League.

Ronaldo aliyepata watoto mapacha hivi karibuni  alipokea tuzo yake mjini London na aliwashukuru mashabiki wake wa Real Madrid, wachezaji wenzake, kocha na rais wake.

Tuzo hiyo kwa mchezaji bora mwanamke imenyakuliwa na mchezaji wa Uholanzi Lieke Martens, anayeichezea Barcelona.

Aliwahi pia kuichezea timu ya taifa ya Uholanzi iliposhinda mashindano ya Euro 2017.


Ronaldo ambaye pia alikumbwa na kashfa ya ukwepaji kulipa kodi amewashinda wachezaji Messi wa Barcelona na Neymar wa PSG

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search