Wakati Wakielekea Kuadhimisha Siku ya Posta Duniani...TPC Wabainisha Kukabiliwa na Changamoto ya Upungufu Wa Watumaji Barua...Soma Habari Kamili na Matukio360...#share

WAKATI Shirika la Posta Tanzania (TPC) likitarajia Oktoba 9 mwaka huu kuungana na Mashirika mengine Duniani Kusherehekea siku ya posta, limesema linakabiliwa na changamoto kubwa ya kupungua kwa kiasi kikubwa watumaji wa barua nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam wakati wakitoa taarifa kwa umma juu ya uwepo wa siku hiyo, Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPC Deo Kwiyukwa, amesema kupukupungua huko si kwa Tanzania pekee bali ni duniani kote.

Aidha amesema hali hiyo inatokana na maendeleo ya teknolojia ya mtandao, alitaja moja wapo kuwa ni mjia ya email. Kutokana na mendeleo hayo yamechangia watu kuhama katika utumaji barua wa kawaida na kutumia njia hiyo.

Katika kukabiliana na changamoto hiyo Meneja Biashara-Barua na Logistics wa TPC Jasson Kalile amesema shirika liliamua kuanzisha huduma ya Posta Mlangoni mfumo ambao unawarahisishia kazi katika kuwahudumia wateja.

Ameeleza huduma hii mteje anapotuma barua, mlengwa wa kupelekewa barua hiyo huipokea mlangoni mwake cha msingi ni mtumaji kuweka anuani ya uhakika.

Amesisitiza kuwa watumaji wa barua kuhakikisha wanaandika anuani za uhakika na pia ametoa rai kwa viongozi wa serikali za mitaa kuandika majina na anuani za wakazi wao wanaoishi maeneo yasiyofikika kwa urahisi ili kuwarahisishia kazi yao ya kuwafikishia barua zao.

Akigusia kuhusu mafanikio waliyopata kama Shirima Mkurugenzi huyo amesema kwamba moja ya mafanikio ni kuboresha huduma kwa umma ikiwa ni pamoja na kuweza kusafirisha baurua na vifurushi kwa haraka.

Akizungumzia shughuli zitakazofanywa siku hiyo ya maazimisho ya siku ya posta duniani, Kwiyuka amebainisha kuwa watatembelewa na wanafunzi ambao watajifunza jinsi shirika hilo linavyofanya kazi zake.

Aidha ameongeza pia watakwenda kutembelea Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) ambapo watawasaidia watoto kwa kuwachangia matibabu, hiyo ikiwa ni sehemu yao katika kuhakikisha wanaifikia jamii.

Pia amesema siku hiyo watatoa Elimu kwa umma ili kuongeza ufahamu wao juu ya shirika hilo pamoja na jinsi ya kulitumia kwa ajili ya maendeleo. 

Na Abraham Ntambara


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search