Wanasiasa washauriwa kuiga mfano viongozi wa dini..Soma habari kamili na Matukio360

Na Hussein Ndubikile

VIONGOZI wa Kisiasa nchini wameshauriwa kuwa wepesi kujenga utamaduni wa kuiga mfano wa viongozi wa dini panapotokea tofauti kwa kutumia njia ya majadiliano ili kupata maridhiano yatakayoendelea kuimarisha na kudumisha umoja na amani ya nchi.

Waziri mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba

Pia wameonywa kuacha kutumia vyombo vya habari kuelezea tofauti zao kwani kufanya kunaweza kuwagawa wananchi na kuhatarisha amani iliyopo.

Hayo yamesemwa leo jijini Dr es Salaam na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambaye pia ni Jaji Mstaafu, Joseph Warioba katika Mdahalo wa Mashauriano Juu ya Umuhimu wa Kuhimiza, Kulinda na Kudumisha Amani na Umoja nchini ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere.

Amesema viongozi wa dini wamekuwa wepesi kukutana kujadili masuala yanayohusu amani ya nchi huku akibainisha suala hilo ni tofauti kwa wanasiasa kwani huvitumia vyombo vya habari kulumbana hata wakati mwinginge kuwagawa wananchi hali inayohatarisha ustawi wa amani.

" Viongozi wa dina wanatusaidia sana kuimarisha umoja na amani  makanisani na misikitini nawaomba wanasiasa muige mfano huu na sio kutumia vyombo vya habari tuache malumbano yasiyo na msingi kwani nchi nyingi zimepata matatizo sababu ya kushindwa kutumia mtindo wa maridhiano, " amesema.

Amebainisha kuwa viongozi wa dini na siasa wana ushawishi mkubwa kwa wananchi hasa pale wanapotumia maneno yanayoweza kujenga au kubomoa amani.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia amesema viongozi hao wanatakiwa kutambua mchango wao katika hivyo waendeleze ushirikano kwa masilahi ya taifa.

Naye Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Nurdin Mangochi ameiomba Serikali kuwasaidia usafiri wa pikpiki, magari na baiskeli ili waweze kuyafikia maeneo yasiyoweza kufikikika kiurahisi na kwamba itasaidia kufundisha mafuundisho mema yenye kuhimiza amani, umoja na upendo.

Amewaasa wanasiasa kufuata misingi ya kuishi kibinadamu ikiwemo ya kuhheshimu rasilamali watu, mamlaka, ardhi pamoja kukubali matokeo yanapotangazwa kuepuka machafuko.

Amefafanua kuwa kinachosababisha wanasiasa kutofautiana ni kutokana na kuwa na mitazamo taofaui ya kivyama huku akisisitiza viongozi wa dini wanahubiri jambo moja ambalo ni umoja na amani.
https://ssl.gstatic.com/ui/v1/icons/mail/images/cleardot.gif




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search