Waziri Dk. Kalemani amsimamisha kazi Meneja uzalishaji umeme...Soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Salha Mohamed

WAZIRI wa Nishati, Dk. Menald Kalemani, amemwagiza Naibu Mkurugenzi Mtendaji Uzalishaji Umeme-Kidatu, Mhandisi Abdalah Ikwasa kumsimamisha kazi Meneja Uzalishaji Umeme, Manfred Ndyalu.

Hatua hiyo imefikiwa kutokana na uzembe wa Meneja huyo kutotoa taarifa za kufyatuka kwa cable katika kituo cha uzalishaji umeme cha Kidatu na kusababisha mitambo mingi hapa nchini kuzidiwa na umeme kukatika.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam alipotembelea maeneo ya uzalishaji umeme Kidatu na Ubungo Dk. Kalemani amesema serikali haiwezi kuwavumilia watu wachache wasiojua majukumu yao.

"Hizo ni hatua za haraka ambazo tunaendela kuzichukua, lakini tunamitambo mingi ambayo haifanyi kazi kama mtambo wa Tegeta haufanyi kazi sawasawa na haujaanza matengenezo,”

"Lakini ni uzembe wa baadhi ya watendaji wetu, lakini pale Kidatu mashine ya Megawat 157 bado haijaanza kufanya kazi kwahiyo nimewaelekeza maeneo yote ambayo hazi Meneja wakuu  wa uzalishaji umeme kuhakikisha mashine zote zinzfanya kazi vinginevyo ajiuzulu mwenyewe,"amesema.

Amesema mfumo unatakiwa kutambua tatizo linapotokea Ubungo  ambacho kimeharibika huku akimtaka Mkurugenzi wa Mfumo na usambazaji kuhakikisha mfumo unaanza kufanya kazi la sivyo ajitafakari kujiuzulu mwenyewe asiporekebisha.

Ameongeza kuwa serikali inahakikisha mitambo yote iliyoharibika inakarabatiwa katika kipindi cha wiki mbili zijazo ili kupatikana umeme usiokuwa na matatizo kama hivi sasa.

Dk. Kalemani amesema kuwa serikali inafanya juhudi kuhakikisha hadi kesho asubuhi maeneo yote ya nchi yanapata umeme huku matengenezo ya kawaida ya kurekebisha mashine ukiendelea kama kawaida.


Amesema Shirika la Umeme (Tanesco), limewataka radhi wananchi kutokana na matatizo yaliyojitokeza huku ikiahidi kurekebisha kasoro zilizojitokeza ili wananchi wapate umeme wa uhakika.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search