Waziri Jafo awapa mtihani wakuu wa mikoa...Soma habari kamili na Matukio...#share

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Selemani Jafo ameagiza kila mkuu wa mkoa nchini kuhakikisha anajenga viwanda vipya 100 katika kipindi cha mwaka mmoja kinachoanzia Desemba 2017.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Selemani Jafo

Kauli hiyo ameitoa leo wakati akizungumza na wakuu wa mikoa wapya walioapishwa juzi na Rais John Magufuli, Jafo amewataka kuitekeleza sera ya ujenzi wa viwanda ipasavyo.

“Lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa ifikapo Desemba 2018 kila mkoa uwe umejenga viwanda vidogo na vya kati visivyopungua 100, mikoa 26 ya Tanzania Bara inatakiwa kuwa na viwanda vipya vidogo na vya kati visivyopungua 2,600 ifikapo Desemba 2018,” amesema Jafo.

Aidha amesema Serikali imekusudia kufikia nchi ya uchumi wa kati kupitia ujenzi wa viwanda huku akiwataka wakuu hao kuibua viwanda vidogo na vya kati kwa kuhamasisha ushiriki wa viongozi ndani ya mikoa na wananchi katika maeneo yao ya utawala.

Jafo ameongeza kuwa, katika kusimamia utekelezaji wa agizo hilo ofisi yake itaweka utaratibu maalumu wa kupima utendaji kazi wa kila kiongozi wa mkoa kwa kuangalia ushiriki wake wa kuwajengea hamasa viongozi wa chini wakiwamo wakuu wa wilaya na wananchi.

Ameeza katika kufanikisha dhana ya ujenzi wa uchumi wa viwanda, Serikali inaendelea kuweka mkazo na kipaumbele katika upatikanaji wa malighafi za kilimo na kuwataka wakuu wa mikoa kuhakikisha kuwa maofisa ugani wanatekeleza vyema majukumu yao ya kazi. 

Kwa upande mwingien Waziri Jafo amewataka wakuu hao wa mikoa kusimamia makusanyo ya fedha za ndani katika halmashauri na kutumia vyema asilimia tano zinazotengwa kuwawezesha wananchi kupata mikopo ili washiriki katika ujenzi wa uchumi wa viwanda.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima amesema ili kufanikisha dhana ya uchumi wa viwanda, Serikali haina budi kuwapa msukumo na ushirikiano wa karibu wanasayansi utakaowezesha kuibua viwanda vingi zaidi pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa malighafi za kilimo nchini.


Mbali na Malima, wakuu wengine wa mikoa waliohudhuria mkutano huo ni Robert Luhumbi (Geita), Joachim Wangabo (Rukwa), Galesius Byakanwa (Mtwara) na Christine Mndeme (Ruvuma).

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search