Waziri Lukuvi apiga 'Stop' bomoa bomoa kwa waliojenga bila vibali...Soma habari kamili na Matukio360..#share
Na Abraham Ntambara
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William
Lukuvi amewataka Maofisa Mipango Miji kutowasumbua kwa kuwabomolea nyumba wananchi waliojenga katika viwanja vyao bila
kuwa na vibali.
Waziri wa Ardhi, Nyomba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza na waandishi wa habari baada ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Nne wa Bodi ya Wataalamu wa Mipangomiji jijini Dar es Salaam.
Pia ameitaka Bodi ya Wataalamu wa Mipangomiji kuandaa
miongozo rahisi ya mipango miji itakayotumika na watendaji wa serikali za mitaa
na vijiji ili kuepusha migogoro mbalimbali ya ardhi nchini.
Kauli hiyo ya Waziri Lukuvu ameitoa leo jijini Dar es Salaam
wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Nne wa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Mipango
Miji, amesema ujenzi bila vibali ni tatizo lililosababishwa na baadhi ya
watendaji wa idara ya ardhi ambao walishindwa kusimamia vyema mfumo huo.
"Kwa sasa hakuna kumsumbua mtu yeyote aliyejenga katika eneo lake halali bila vibali, hii ni kwa sababu serikali yenyewe kupitia watendaji wake walishindwa kusimamia vizuri, lakini kinachotakiwa pia kwa wale waliojenga makazi holela wanatakiwa kupimiwa na kurasimishwa ardhi," amesema Lukuvi.
Amesema kwanzia sasa ni marufuku kwa Maofisa wa Mipango Miji
kuwasumbua wananchi hao, isipokuwa wale waliojenga makazi holela wanatakiwa
kupimiwa na kurasimishwa maeneo yao ili waweze kuyamiliki kihalali kwa mujibu
wa sharia.
Akizungumzia kuhusu kukosekana kwa miongozo rahisi katika
ngazi za mitaa na vijiji, amesema inachangia kuwepo kwa mipango miji mibovu na
kuongeza kuwa miongozo hiyo itasaidia watendaji wa mitaa na vijiji kusiamia
zoezi la upangaji wa miji ambalo linanafanyika ndani ya miaka 10 kwa nchi nzima.
Ameongeza kuwa serikali imeamua kuzipa kipaumbele Kampuni za
ndani katika kusimamia zoezi la upangaji miji kutokana na kwamba zimekuwa
zikifanya kazi nzuri na kwa gharama ya chini.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi hiyo Profesa Wilbard Kombe
amesema tasnia ya mipangomiji bado ni changa kwa maana kwamba wataalam wa
mipanomiji ni wachache ukilinganisha na
mahitaji.
“Tafiti zinaonyesha kuwa wataalamu waliopo ni asilimia 25 tu
ya mahitaji. Pamoja na hayo, kati ya wataalamu takribani 700 wenye taaluma ya
mipangomiji ni wataalamu 306 tu waliosajiliwa hadi sasa,” amesema Prof. Kombe.
Aidha ameongeza kuwa zipo mamlaka za upangaji ambazo
haziajiri wataalamu wa Mipangomiji na kupelekea baadhi ya Halmashauri kukosa
wataalamu hao, huku Sheria ya Mipangomiji No 8 ya mwaka 2017 ikizitaka
Halmashauri zote kuwa na wataalamu wa Mipangomiji aliyesajiliwa na bodi.
Ameomba Halmashauri zote nchini kuhakikisha zianaajiri
wataalamu wa mipangomiji waliosajiliwa au kuhimiza waliopo kusajiliwa kama
wanazo sifa za kusajiliwa.
No comments:
Post a Comment