Waziri Ummy-Hospitali za serikali pimeni saratani kizazi na matiti kila mwezi...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Salha Mohamed
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu  amezitaka hospitali, zahanati na vituo vya afya ngazi ya wilaya kila mwezi  kutenga siku moja  kupima saratani ya shingo ya mlango wa kizazi na matiti.
Waziri Ummy Mwalimu akihutubia mara baada ya kumaliza matembezi ya kuhamasisha upimaji na kuchangia damu kwa wagonjwa wa saratani jijini Dar es salaam leo 

Wito huo ameutoa leo jijini Dar es Salaam  mara baada ya kuhitimisha matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa saratani ya matiti na saratani ya shingo ya mlango wa kizazi katika viwanja vya Taasisi ya saratani Ocean Road.

Amesema  ugonjwa wa  saratani unaongezeka kila takwimu za wizara ya Afya zinapotolewa na kila mwaka kuna wagonjwa wapya wa saratani 50,000.

"Ikifika 2020  wagonjwa na vitu vitokanavyo na saratani vitaongezeka mara mbili ya wagonjwa wapya na kufikia wagonjwa 100,000 kama hatua hazitachukuliwa, "amesema.

Waziri Ummy amesema kutokana na takwimu hizo ni asilimia 26 ya wagonjwa ndiyo hufika hospitali kwa ajili Uchunguzi wa saratani.

Amesema katika wagonjwa 100 wagonjwa 74 hawajulikani wanapopata tiba na uchunguzi huku asilimia 80 ya wagonjwa hufika wakiwa katika hatua za mwisho na kusababisa matibabu kutokuwa mazuri.

"Saratani tunaweza kushindwa,  leo tumetembea kuonesha hamasa na tumeokoa maisha ya watu wengi na serikali imeandaa mkakati wa kuondoa saratani kabisa, "amesema Waziri Ummy.

Ameongeza awali upatikanaji wa dawa ulikuwa asilimia 4 tu kutokana na bajeti ndogo nakusababisha upatikanaji wake kuwa mgumu kwa kupokea milioni 790 kwa mwaka 2005/2017 lakini  bilioni 7 kwa mwaka 2016/2017 zimetolewa.

Amesema kutokana na ukubwa wa tatizo serikali itashusha zaidi dawa ili kutibu wagonjwa wengi zaidi.

Amesema kwa sasa mgonjwa anatakiwa kupata huduma ya matibabu ndani ya wiki mbili na si wiki sita kama ambayo Mkurugenzi wa Taasisi hiyo,Dk.  Julius  Mwaiselage alivyosema.

Ummy amesema serikali inataka hadi kabla ya June 30, 2018  kuwa na kipimo cha kisasa Afrika Mashariki kwani itapunguza wagonjwa wa nje kwa kufuata kipimo cha PET/CT Scan ambapo imetoa bilioni 14.5.

Amesema hadi kufikia Desemba 2018 wawe wamepima wagonjwa 3,000,000 pamoja na kutoa elimu kwa wanafunzi wa shule za msingi.

Kwa upande wake Dk Mwaiselage amesema saratani ikiwahi kutibiwa inatibika na kuwa elimu zaidi inahitajika.

"Mashine mbili mpya zitafungwa na itapunguza muda wa kusubiri tiba na hata wanaotaka kwenda nje ya nchi, "amesema.

Ameongeza kupitia matembezi hayo wameboresha wodi ya Chemotherapy(tiba kwa drip)  kutoka vitanda 40 hadi  100. 
           




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search