Kampuni 500 kushiriki maonesho nchini...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Abraham Ntambara

ZAIDI ya kampuni 500 yanatarajia kushiriki katika maonesho ya pili ya bidhaa za viwanda  yatakayofanyika kuanzia Desemba 7 hadi 11, 2017 katika uwanja wa maonesho wa mwalimu J.K Nyerere.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage akizungumza na waandishi wahabari jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam juu ya maandalizi ya maonesho hayo, Waziri wa Viwanda na Biashara Charles Mwijage amesema katika maonyesho ya mwaka jana ni makampuni 472 pekee ndiyo yaliyoshiriki.

“Lengo kuu la maonesho haya ni kujenga jukwaa kwa wadau wa viwanda kupata fursa ya kujadiliana, kubadilisha uzoefu na kutangaza biashara za watanzania wote wanaomiliki viwanda vidogo, vya kati na vikubwa,” amesema Mwijage.

Mwijage amesema maonesho hayo mwaka huu yanabeba kauli mbiu isemayo “Tanzania sasa tunajenga viwanda” ikilenga kuwaaminisha wananchi juu ya falsafa na dhima ya ujenzi wa viwanda wa uchumi wa viwanda.

Ameongeza, meonesho hayo yatawakutanisha wadau wa viwanda ikiwemo wazalishaji wa malighafi, taasisi zinazotoa huduma mbalimbali kwa wenye viwanda na taasisi zinazowezesha wenye bidhaa kutoka kiwandani mpaka kufikia kwa mtumiaji.

Amesema wakati wa maonesho Desemba 11, 2017 itakuwa siku maalumu ya viwada Afrika ambayo itaratibiwa na kwa ushirikiano na Taasisi za Umoja wa Mataifa ya Maendeleo ya Viwanda (UNIDO).

Waziri Mwijage amesema wizara yake kupitia Mamlka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade) imewakaribisha watanzania wanaomiliki viwanda vidogo, vya kati na vikubwa kushiriki maonesho hayo.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search