Lukaku avunja rekodi upachikaji mabao timu ya taifa...soma habari kamili na Matukio360..#share

MSHAMBULIAJI wa timu ya Taifa ya Ubelgiji na Manchester United  Romelu Lukaku, ameweka rekodi ya ufungaji wa magoli mengi katika timu ya taifa hilo.
Romelu Lukaku
Timu ya Ubelgiji inayofundishwa na Roberto Martinez waliifunga jana Japan bao 1-0 huko Brugge.
Lukaku, 24, alifunga goli hilo na kufikisha mabao 31 akiwa mchezaji wa kikosi hicho.
Mshambuliaji huyo  alimalizia krosi safi kutoka kwa Nacer Chadli aliyoiingiza wavuni kwa kutumia kichwa.
Kabla ya kufunga goli hilo, Lukaku alikuwa sawa  na wachezaji Bernard Voorhoof na Paul van Himst kwa kuwa na magoli 30 kila mmoja.
Ubelgiji waliendeleza msururu wao wa kutoshindwa hadi mechi 15.
Mara yao ya mwisho kushindwa ilikuwa mikononi mwa Uhispania mechi ya kirafiki Septemba 2016.
Katika michezo mingine iliyochezwa jana, Uholanzi walipata ushindi wao wa pili tangu kukosa nafasi ya kushiriki katika Kombe la Dunia nchini Urusi walipopokeza Romania kichapo cha magoli 3-0 huko Bucharest.
Mshambuliaji wa zamani wa Liverpool Ryan Babel alifunga bao lake la kwanza la kimataifa tangu mwezi Mei 2008, pamoja na mchezaji mwenza Memphis Depay na Luuk de Jong.
Mabingwa wa Euro 2016 Ureno walitoka sare 1-1 na Marekani, wakicheza bila nyota wao Cristiano Ronaldo. Vitorino Antunes alikomboa bao lililokuwa limefungwa na Mmarekani Weston McKennie mapema mwenye mechi Leiria.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search