Nyalandu amjibu Waziri Dk. Kigwangalla...Soma habari kamili na Matukio360...#share
SAA chache baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Hamisi
Kigwangalla kumzungumzia aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini kwa tiketi ya
Chama cha Mapinduzi (CCM) Lazaro Nyalandu, amemjibu kuwa anatumika.
Nyalandu kupitia ukurasa wake wa Facebook amemjibu kama ifuatavyo..
INASIKITISHA sana kuona WAZIRI Kigwangalla akitumia MUDA wake
ndani ya BUNGE leo kunichafua, kunidhihaki, na kusema UONGO na UZUSHI dhidi
yangu, ikiwa ni NJAMA za makusudi zilizopangwa kunichafua mara baada ya mimi
kukihama Chama Cha Mapinduzi -CCM. Aidha, hatua hiyo imepangwa kwa lengo la
kuhakikisha kuwa hakuna kiongozi yeyote wa CCM atakayethubutu ama kudiriki tena
kukihama Chama Cha Mapinduzi CCM katika Serikali hii ya awali ya tano. AIDHA,
Waziri Kigwangalla anatumika VIBAYA, kwa kauli za UONGO na UZUSHI aliuanza
DHIDI yangu mara tu alipoteuliwa, kwa kuanza kutoa kauli za kejeli dhidi ya
UTUMISHI wangu uliotukuka ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii na wenye
REKODI thabiti.
NIANZE na UZUSHI alioutoa Waziri Kigwangalla mapema leo BUNGENI,
huku moyoni mwake akiwa anajua fika kuwa ametumwa kusema UONGO dhidi ya Waziri
Nyalandu kwa lengo la kuandaa MAZINGIRA ya kumkamata na kubwa zaidi,
kudhalilisha azma ya WATANZANIA ambao WAKO tayari kwa mabadiliko ya UONGOZI wa
nchi kupitia UPINZANI. AIDHA, propaganda za Kigwangalla ameamua zimuhusu Waziri
moja tu wa Maliasili, tangu TAIFA kupata Uhuru. Waziri huyu ni Nyalandu, ambaye
wala sio Waziri ambaye yeye amemrithi alipoteuliwa kuwa WAZIRI, jambo
linalothibitisha NJAMA na Progaganda za kuzimisha MOTO na nguvu ya umma kupitia
UPINZANI, hasa baada ya kitendo changu Cha kukihama CCM.
1) WAZIRI Kigwangalla amekejeli kuwa Waziri Nyalandu alitumia
Fedha za Serikali kusafiri USA na mwanadada Aunt Ezekiel.
-HABARI hii ilikuwa ya KUZUSHA na ilichunguzwa na vyombo vya dola 2014 na
kuthibitika ilitungwa na ilikuwa ya UONGO. Katika Mkutano huo wa Washington,
DC, Waziri Nyalandu alialikwa na Balozi wa Tanzania, Marekani, na alipewa
RUHUSA ya maandishi na Serikali kuhutubia Mkutano huo kwa siku Moja. Wasanii
wote
Walioalikwa, akiwepo Mwanadada Aunt Ezekiel, hawakuwa na mwaliko wa Wizara ama
Serikali, bali waandaji wa Kongamano. Na Serikali haikulipa gharama zozote
kwao.(Mthibiti
Na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali anaweza kuthibitisha)
2) Waziri Kigwangalla amedanganya BUNGE kuwa Waziri Nyalandu
alitumia helikopta kugombea URAIS 2015.
-Habari hii ni ya uzushi na UONGO, na Waziri atakuwa aidha hana BUSARA ambayo
angepaswa kujiridhisha na Taarifa kabla ya kuisoma Bungeni, ama waliomtuma
wamemwambia ASOME TU hivyo hivyo. UKWELI ni kuwa, Waziri Nyalandu, alipokuwa
CCM, aligombea katika kinyang’anyiro cha URAIS kuomba kuteuliwa ndani ya CCM,
na alitumia aidha usafiri wa MAGARI au NDEGE za kawaida kwa kulipa nauli (fixed
wings pale ilipobidi), hadi mchakato ulipoisha kama uilivyoisha.
-AIDHA, miaka yote nikiwa Mbunge wa Singida Kaskazini, nimekuwa
nikifanya kampeni za kumalizia kwa njia ya helikopta. Inawezekana Waziri
Kigwangalla hajawahi kupanda helikopta katika maisha yake, nimjulishe TU kuwa
kwangu huo ni usafiri wa kawaida sana na umesaidia ilipobidi kusaidia kufika
baadhi ya maeneo Jimboni kwangu wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu 2000, 2005,
2010, na 2015.
-AIDHA, Mwaka 2015 nilitumia Helicopter kwa SIKU TATU za kumalizia Kampeni, na
nilikodi helikopta hiyo kwa Sh milioni tano kwa siku (Jumla, milioni 15)
-Pia ingependeza kama hamaki za Kigwangalla zingemkumbusha kuwa Waziri Nyalandu
akiwa Wizarani ALIPATIA Serikali Helikopta mpya Moja, alileta ndege kwa
matumizi ya kupambana na Ujangili, Alishawishi Benki ya dunia, Ujerumani na USA
kuleta mamilioni ya dola za kmarekani kusaidia mapambano hayo, na kwamba
alifanikiwa Sana kutokmeza ujangili nchini. RAIS KIKWETE alikiri hili wakati wa
kuzindua Tangazo la Tanzania (Tanzania, the soul of Africa).
3) Kigwangalla amezusha kuwa Waziri Nyalandu alitumia vibaya
madaraka yake. Amezungumzia suala la Waziri Nyalandu kutotia sahihi TOZO mpya
zilizopendekezwa na TANAPA. Jambo ambalo Waziri Kigwangalla angepaswa kulijua
kabla ya kutoa kauli isiyo sahihi Bungeni ni kuwa SAKATA la TOZO za Tanapa
lilijadiliwa BUNGENI mbele ya Spika Mama Anne Makinda, likiwa limeletwa na
Kamati ya Lembeli, na kwa kupitia Wizara, Waziri Nyalandu alilitolea ufafanuzi
na likamalizika na GN ilitolewa.
-SAKATA la kupandishwa ghafla kwa TOZO za mahotelini zinazojulikana kama (Fixed
Rates) lilianza kabla sijawa Waziri. Aidha, kulikuwa na kesi Mahakama Kuu,
ambako hadi kufikia mwaka 2012, uamuzi wa Mahakama uliyotolewa. Bado Nyalandu
hakuwa Waziri. Aidha, nilipoteuliwa kama Waziri, Nikatazama SAKATA hilo ambalo
lilishachukua muda mrefu sana hadi kufikia 2014, mimi nilipokuwa Waziri. Sheria
inasema ”Concession Fees shall be 10% of half Board”, na kulikuwa
Na GN ya Serikali kuhusu TOZO hizo, takribani kuanzia mwaka 2002. Hukumu ya
Jaji wa Mahakama Kuu ilielekeza kuwa TOZO zozote mpya ni sharti zipate GN mpya,
na sheria ya msingi ilitaka TOZO ziwe kwa asilimia (percentage), na sio TOZO za
kukisia, (fixed rate) ambazo ndio msingi mkubwa wa kupendeleana na rushwa
katika kupanga nani alipe kiwango gani Cha kodi. Baada ya kuitolea maelezo
Bungeni (na hansardi Zipo), Bunge na Wizara tulikubaliana namna ya kulimaliza
na ndivyo ilivyofanyika na GN ilitolewa. Waziri Kigwangalla hajasema ukweli na
amezusha kuhusu suala hili kwa sababu anazozijua mwenyewe.
4) Sakata la VITALU: Inasikitisha SANA na inatia AIBU kwamba
Waziri atalihadaa BUNGE kwamba Waziri Nyalandu amehusika na kuuza VITALU au
kugawa VITALU, na baya Zaidi kwa NJIA ya RUSHWA.
-Sheria ya Wanyamapori inatamka wazi kuwa VITALU vitagawiwa kwa wawindaji kwa
kila baada ya miaka MITANO.
-Mara ya mwisho VITALU vimegawiwa Januari, 2017. Nyalandu hakuwa WAZIRI.
(Waziri alikuwa Mh. Prof Maghembe)
-Kabla ya hapo, VITALU viligawiwa mwaka 2013. Nyalandu hakuwa Waziri. (Waziri
alikuwa Mh Maige)
Hii ni AIBU sana na natumaini kwa Waziri Kigwangalla na wanaomtuma wangetamani
sana miaka ibadilike ili isomeke Waziri Nyalandu.
5) Waziri Kigwangalla amedai kuwa Waziri Nyalandu alikuwa
anafanyia Kazi katika Chumba maalumu katika hoteli ya Serena. Naomba Waziri
Kigwangalla, athibitishe ni Chumba namba ngapi, na wahusika wa hoteli pia
wathibitishe. Kama Waziri, nilifanya Kazi katika ofisi yangu iliyopo Wizaranya
Maliasili na Utalii. Kigwangalla pia akumbuke mimi nilikuwa MTEULE wa Rais
ambaye alikuwa na vyombo vya kumsaidia kusimamia Mawaziri.
6) Mbwembwe hizi na kusingiziwa kunakofanywa kwa makusudi baada
ya mimi Nyalandu kukihama CCM ni aibu kwa TAIFA na ni matumizi mabaya sana ya
MADARAKA. Aidha, ifahamike kuwa Vitisho na njama dhidi yangu na familia yangu
kunakofanywa na wote wanaohusika hakutazimisha azma ya watanzania kutaka
mabadiliko ya kweli nchini. Imeandikwa, WAONGO wote, sehemu yao ni katika ziwa
liwakalo moto kwa kiberiki. Haki huinua Taifa, na uonevu na dhuluma ni dhambi
itakayowatafuna wahusika siku zote za Maisha yao.
Lazaro S. Nyalandu




No comments:
Post a Comment