Ununuzi nyumba za Lugumi utata!...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na  mwandishi wetu
UTATA umegubikwa kuhusu ununuzi wa nyumba za mfanyabiashara Said Lugumi zilizouzwa kwa njia ya mnada hivi karibuni.

 Moja ya nyumba ya mfanyabiashara, Said Lugumi iliyouzwa hivi karibuni kwa njia ya mnada

Habari zilizopatikana ni kuwa mnunuzi wa nyumba hizo Dk Luis Shika amedaiwa kuwa ni tapeli na kwamba  inadaiwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi.

Hata hivyo kamanda wa polisi kanda maalumu  ya Dar es Salaam, SACP Lazaro Mambosasa  leo ameiambia Matukio360 kuwa hana habari za kukamtwa kwa mununuzi huyo, Dk Shika

"Hadi muda huu(saa nane na nusu mchana) bado sijapata taarifa zozote kuhusu kukamatwa kwa huyo mnunuzi. Natumai hadi kesho ninawezakuwa na taarifa kamili kuhusu hilo," amesema Mambosasa



Inadaiwa kuwa nyumba ya Lugumi iliyopo JKT Mbweni imenunuliwa kwa bilioni 1.1 na nyingine kwa bilioni 1.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search