'UPDATES' Mtoto wa Chacha Wangwe jela mwaka mmoja na nusu...soma habari kamili na Matukio360..#sgare

Na Abdulrahim Sadiki

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu  leo imemtia hatiani na kumuhukumu kwenda jela mwaka mmoja na nusu au kulipa faini ya milioni tano, BOB Chacha Wangwe ambaye ni  mtoto wa mwanasiasa marehemu Chacha Wangwe.



 Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Hatua hiyo inafuatia baada ya hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo, Huruma Shaidi kuridhika na ushahidi uliotolewa kuwa Bob Chacha kuchapisha taarifa za uongo kwenye mitandao ya kijamii

Upande wa Mashtaka uliwaita mashahidi sita kutoka ushahidi kwenye kesi hiyo na mshtakiwa huyo kujitetea mwenyewe

Kwa mujibu wa kesi hiyo  namba 167, 2016 ambayo ilifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Mei 12,2016.

Bob Chacha Wangwe ambaye kitaaluma ni mwana sheria na mwanaharakati wa haki za binadamu anadaiwa kutenda kosa la kuchapisha taarifa za kupotosha katika ukurasa wake wa Facebook.


Mshtakiwa huyo anadaiwa kutenda kosa hilo Machi 15,2016 na kwamba alichapicha maneno haya; “Tanzania ni ambayo….inajaza chuki wananchi … matokeo ya kubaka Demokrasia Zanzibar ni hatari zaidi ya muungano wenyewe…. Haiwezekani nchi ya Zanzibar kuwa koloni la Tanzania bara kwa sababu za kijinga.”


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search