‘UPDATES’ Wapigania uhuru Zimbabwe wampa siku tatu Mugabe ajiuzulu urais..soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mashirika ya kimataifa
SAA chache baada  chama tawala nchini Zimbabwe Zanu-PF kimemfuta Robert Mugabe kama kiongozi wake na Grace Mugabe ambaye alikuwa mwenyekiti wa taifa wa wanawake, wapigania uhuru wa nchi hiyo wamempa siku tatu Mugabe ajiuzulu urai kwa hiari yake.

Msimamo huo umetangazwa  leo muda huu na mkuu wa chama chenye nguvu cha wale waliopigania uhuru, Chris Mutsvangwa.


Ameiambia Reuters kuwa chama  kinaanza mchakato wa kumuondoa Mugabe madarakani kama rais endapo atakataa kujizulu mwenyewe.

"Tumempa siku tatu ajiuzulu mwenyewe akishindwa kutekeleza hilo, tutamtoa kwa nguvu,’’ amesema Chris Mutsvangwa..

Zanu-PF ndio chama kilichomsaidia Mugabe kuwa madarakani nchini kwa takriban miaka 40.
Lakini sasa inabidi wamshinikize ajiuzulu kufuatia mpasuko mkubwa katika chama tawala.

Pia Zanu-PF kimemfuta waziri wa elimu  Jonathan Moyo na waziri wa serikali za mitaa, Saviour Kasukuwere

Kimemteua aliyekuwa makamu wa rais, Emmerson Mnangagwa ambaye alifutwa wiki mbili zilizopita kama kiongozi wake.

Hata hivyo kufutwa kwa  Mnangawa kumezua mambo mengi huku jeshi likitwaa madaraka na kumzuia Mugabe mwenye umri wa miaka 93, kumteua mke wake, Grace kama makam wa rais.

Jana waandamanaji walipiga kambi nje ya makao ya Mugabe kumshinikiza kujiuzulu

Maelfu ya watu nchini Zimbabwe waliingia barabarani siku ya Ijumaa kuandamana kumpinga  Mugabe.
Mugabe anatarajiwa kukutana na makanda wa jeshi na msafara wa magari umeonekana ukiondoka makao ya rais.

Jeshi la nchi hiyo lilichukua hatamu za kiserikali na kumweka Mugabe chini ya kizuizi cha nyumbani tangu juzi na wamekuwa wakifanya mazungumzo ya kina.


Mugabe angependelea mkewe kumrithi lakini wapiganiaji wa uhuru nchini humo wanamtaka aliyekuwa makamu wa Rais Emmerson Mnangagwa ambaye Mugabe alimfuta kazi wiki iliyopita, kutokana na uhasama mkubwa baina yake na mkewe rais Mugabe uliotokana na upiganiaji huo wa madaraka.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search