Wawili wajiondoa kugombea udiwani ....soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
WAGOMBEA wawili wa udiwani, Lunda Rashid Ulaya(CHADEMA) kata ya Milongodi wilayani Tandahimba mkoani Mtwara  na Juma Mohamed Siyame wa  Chama cha ACT Wazalendo kutoka kata ya Ndalambo katika Halmashauri ya Momba. wamejiondoa katika kinyanganyiro hicho
Watendaji wa wakuu wa NEC

Taarifa hiyo inasema
"Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeridhia kujitoa kwa wagombea wawili wa Udiwani katika Kata ya Milongodi, Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba Mkoani Mtwara na Kata ya Ndalambo katika Halmashauri ya Wilaya Momba  mkoani  Songwe.
Wagombea  waliojitoa ni Ndugu Lunda Rashid Ulaya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kutoka katika kata ya Milongodi Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba na Juma Mohamed Siyame wa  Chama cha ACT Wazalendo kutoka kata ya Ndalambo katika Halmashauri ya Momba.

Katika kikao cha chake kilichofanyika tarehe 14/11/2017 jijini Dar es Salaam, Tume imeridhia  uamuzi wa kujiondoa kwa wagombea hao wawili katika nafasi ya udiwani, baada ya kukamilisha taratibu zote za kujitoa.

Miongoni mwa taratibu hizo ni mgombea kuandika barua kwa msimamizi wa uchaguzi wa jimbo au msimamizi msaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata kumjulisha uamuzi wa kujitoa .

Katika barua yake kwenda kwa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Kata, mgombea wa kata ya Milongodi Ndugu Lunda Rashid Ulaya katika barua yake ya tarehe 4/11/2017 hakueleza sababu zilizomfanya ajitoe kwenye kinyang’anyiro hicho cha kugombea udiwani.

Kwa upande wake mgombea wa ACT WAZALENDO Ndugu Juma Mohamed Siyame, katika barua yake ya tarehe 10/11/2017 alieleza sababu za kujitoa  ni kuwa na majukumu ya kifamilia na hivyo asingeweza kumudu kuwatumikia wananchi wa Ndalambo katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Kutokana na kujiondoa kwa wagombea hao, idadi ya wagombea waliobaki katika kinyang’anyiro hicho sasa ni 151. Uchaguzi mdogo wa madiwani unafanyika katika kata 43 ambazo ziko katika Halmashauri 36   kwenye mikoa 19   Novemba 26, 2017.

Imetolewa leo tarehe 15 Novemba, 2017 na:-

Kailima, R.K
MKURUGENZI WA UCHAGUZI



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search