Achoma nyumba na kumuuwa mume wake....soma habari kamili na matukio360..#share

Na Mwandishi Wetu, Mtwara

JESHI la Polisi Mkoani Mtwara linamsaka  Zuhura Ismail (29) kwa tuhuma za kumuua mume wake baada ya kumfungia ndani na kuichoma nyumba kwa petroli.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Lucas Mondya.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kamanda wa Polisi mkoani humo Lucas Mkondya, amesema kwamba chanzo cha tukio hilo ni wivu wa mapenzi,  baada ya mwanamke huyo kugundua mume wake anaishi na mke mwingine hivyo akaamua kumvizia nyumbani kwake na kuichoma moto.

"Ni kweli Jeshi la linamsaka mwanamke mmoja ayefahamika kwa jina la Zuhura Ismail kwa tuhuma za kuichoma nyumba aliyokuwa anaishi mume wake na mwanamke mwingine, kutokana na wivu wa kimapenzi baada ya Zuhura kugundua kuwa mumewe anaishi na mke mwingine," amesema Kamanda Mkondya.

Ameeleza kuwa moto huo uliwasababishia majeraha makubwa  na kukimbizwa hospitali lakini kutokana na majereha hayo makubwa alifariki dunia huku mwanamke aliyekuwa nae akiendelea vizuri.

Kamanda Mkondya amesema mara baada ya tukio hilo Zuhura  alitoroka na kwenda kusikojulikana na Jeshi la Polisi linaendelea kumsaka na pindi atakapopatikan atafikishwa katika vyombo vya sheria.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search