LHRC: Nchi inapita katika hali ngumu...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara

KITUO cha sheria na haki za binadamu (LHRC), kimesema nchi kwa sasa inakabiliwa na hali mbaya kwenye haki za kisiasa, kiraia na uhuru wa vyombo vya habari  kuliko kipindo chochote kuwahi kutokea nchini.
Mkurugenzi mtendaji wa kituo cha sheria na haki za binadamu (LHRC) Dk Hellen Kijo Bisimba akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam. 

Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Dk. Hellen Kijo Bisimba ameeleza hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika sherehe za kuadhimisha siku ya kimataifa ya haki za binadamu inayoanzimishwa kila  Desemba 10 na kwamba wameazimisha jana ili kuipisha serikali itakayoadhimisha Desemba 10 .

“Kama nchi tunamatatizo makubwa  kwenye haki za kisiasa, kiraia na uhuru wa vyombo vya habari,” amesema Dk. Kijo Bisimba.

Ametaja haki hizo nkuwa kutokuwapo kwa  mikusanyiko ya kisiasa, maandamano, kujieleza na uhuru wa kupata habari na kuripoti kwa upande wa vyombo vya habari.

“Juzi juzi tulikuwa na mkutano na waandishi wa habari tulivyomaliza tu vyombo vilivyotoa taarifa vikaitwa na mamlaka ya mawasaliano nchini (TCRA) kwa ajli ya kujieleza kwa nini wametoa zile habari,” ameeleza.

Hata hivyo ameipongeza serikali katika kupambana na  kudhibiti vitendo vya rushwa  na ubadhilifu wa mali za umma na kwamba vimeanza kupungua.


Amesema lengo la maadhimisho hayo ni  kujitathimini na nini kifanyike kuhakikisha haki za binadamu zinaendelea kulindwa na kuheshimiwa.



"Baada ya majadiliano, tutapelekea mapendekezo yetu kwa lengo la  kuishauri serikali nini chakufanya ili nchi iendelee kuwa salama katika kipindi cha mpito cha mkakati wa kuelekea uchumi wa viwanda vya kati,'' amesema.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search