Prisons kuongeza wachezaji watatu...soma habari kamili na matukio360...#share


Yusta Nkwelengushe, Mbeya

UONGOZI wa Tanzania Prisons umesema katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo utaongeza wachezaji watatu na hautaacha mchezaji hata mmoja. 
Timu ya soka ya Prisons

Prisons yenye kikosi cha wachezaji zaidi ya 25 inaendelea na mazoezi katika uwanja wake wa Magereza kwa ajili ya kuhakikisha inaendeleza rekodi ya kufanya vizuri katika michuano ya Ligi Kuu Bara inayotarajia kuendelea wiki ijayo.


Katibu wa klabu hiyo, Havintish Abdallah amesema  nafasi hizo ni kiungo, golikipa na nafasi nyingine moja ya ziada ili kuwa na wachezaji wa kutosha .

Amesema kwa sasa hawezi kuweka wazi majina na timu wanazotoka wachezaji hao kutokana na kukwepa ‘figisu’ za kuchukuliwa na timu nyingine.

Taarifa za uhakika ambazo mwandishi amezipata ni kwamba  uongozi wa maafande hao umepenya jicho lake Zanzibar walikoweka kambi kabla ya kuanza kwa pazia la ligi msimu huu.

Abdallah amesema “Tupo katika mchakato huo na mazungumzo yetu na wachezaji tunaowahitaji  yanakwenda vizuri na muda wowote tunawasainisha kandarasi ya kuungana na wenzao katika kulisukuma gurudumu hili’’.

Amesema ingawa wana kikosi cha wachezaji zaidi ya 25 lakini wameona ni vyema wakaongeza nafasi hizo tatu kutokana na ugumu wa ligi unavyoonekana.

‘’Ligi ni ngumu kwa hiyo kipindi hiki tunatumia kuboresha kikosi ili tuweze kupambana kikamilifu na kuweza kumaliza ligi katika nafasi nzuri,’’amesema Abdallah


Tanzania Prisons inashika nafasi ya sita kimsimamo kati ya timu 16 zinazoshiriki ligi ikiwa imevuna pointi 15 baada ya kucheza mechi 11 ikiwa imefungwa mechi  mbili,kutoa sare sita pamoja na kushinda mechi tatu.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search