Lukuvi kukutana na wataalam wa ardhi...soma habari kamili na matukio360..#share



Na Heri Shaaban, Dar es salaam

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi anatarajia kuwa mgeni rasmi katika mkutano wa mwaka wa wataalam wa ardhi  waliosoma chuo cha ardhi Morogoro .

I
Waziri wa ardhi, William Lukuvi

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, mwenyekiti wa wataalam waliosoma chuo cha ardhi  Morogoro, Salum Shaka amesema  mkutano huo unatarajiwa kufanyika mwezi  Machi,  2018 ikiwa ni  mwendelezo wa mikutano ya umoja huo  inayofanyika kila mwaka.

"Umoja wa wataalam waliosoma  chuo cha ardhi Morogoro tumeweka utaratibu kila mwaka  tunafanya tathimini na kujadili maendeleo ya umoja wetu," amesema Shaka

Amewataka wataalam wote  ambao wamesoma chuo hicho  wajitokeze  kuzungumza na waziri  katika viwanja vya chuo hicho.

" Siku hii ni maalum kwetu ambapo mwanzoni mwa machi  2018 tutakutana mambo mbalimbali  ya chuo yatajadiliwa kwa lengo la kupanua wigo  wataalam kwa wataalam kujenga uwezo katika utendaji wa majukumu yetu  na kujenga weledi wakiwa kazini," amesema.

Amesema siku  hiyo ni maalum kwa kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu sekta ya ardhi.

Amesema kwa sasa nchi  inaelekea kwenye uchumi wa kati  na kauli mbiu siku hiyo ni "Ardhi  ni msingi  mkuu kufikia azma ya Tanzania ya Viwanda."

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search