Makalla atengua maamuzi ya mkuu wa wilaya....soma habari kamili na matukio360..#share


Na mwandishi wetu, Mbarali
MKUU wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla ametengua agizo la mkuu wa wilaya ya mbarali na kuagiza wakulima waendelee kulima mazao  yao hususan  mpunga kwa kutumia skimu ya umwagiliaji maji.

Mkuu wa Mkoa Amos Makalla(katikati) akiangalia namna uharibifu wa mazingira uliofanywa kwenye kingo za mto Mbarali kutokana na shughuli za kilimo cha umwagiliaji kusho) kwake ni mkuu wa  wilaya hiyo, Reumen Mfune.

Hivi karibuni mkuu wa wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune aliagiza kufungwa kwa skimu ya umwagiliaji ya mnazi iliyopo katika kata ya Imalilo Usongwe kwa madai ya kuharibu vyanzo vya maji vya mto ruaha.

Lakini jana katika mkutano wake wa hadhara uliofanyika katika kata ya Imalilo Usongwe, Makalla ameagiza  kuchimbwa mfereji wa skimu uliokuwa umefukiwa na kwamba serikali wilayani humo ndio iliyoshindwa kuhusimamia na kuweka sawa miundombinu ya umwagiliaji kwa wakulima.

Amesema licha ya wakulima  kutumia  mfereji huo bila kibali,changamoto iko kwa serikali kwa kuwa haikuandaa mipango ya kuboresha miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji .

Makalla amesema kitendo cha  kufunga mfereji kunaweza kusababisha   zaidi ya hekari 5,700   kutolimwa katika msimu huu wa kilimo na takribani  wakulima 2,000 wanaweza kukosa   chakula  suala ambalo ni hatari kwa taifa.

"Kuanzia leo(jana) kaendeleeni na shughuli za kilimo pia  toeni ushirikiano kwa  viongozi wa halmashauri kufukua mfereji  na sipendi kusikia kuna tofauti au kuwepo kwa vitendo vya  kuwakwaza wananchi katika zoezi hilo,"alisema Makalla.

Amesema uchumi wa viwanda hauwezi kufanikiwa kama wakulima watakosa sehemu ya kuzalisha mazao kwa sababu ya ukosefu wa maji.
“Kimsingi kosa lilifanywa na Serikali kwa kutoandaa mazingira rafiki  na ndio tumefikia hatua hii,’’ amesema.

Awali mkuu wa wilaya ya Mbarali,  Reuben Mfune, alieleza sababu ya kufungwa kwa skimu hiyo ni kutekeleza  agizo lililotolewa na kikosi kazi kilichondwa na makamu wa rais, Samia Suluhu kutokana uharibifu unaofanywa katika  hifadhi ya mto ruaha kunakosababishwa na shughuli za kilimo cha umwagiliaji .

Mbunge wa jimbo la Mbarali (CCM) Haroon Mulla, alipongeza maamuzi ya mkuu wa mkoa  huyo wa kwamba amekuwa akichukiwa na wananchi wake kutokana na chokochoko za kisiasa.

"Wananchi  mnanichukia bure ninatambua kuna jinamizi limepita ambalo linanichonganisha na nyinyi mimi nimepigania  sana suala la kufungwa kwa  skimu hiyo   kwa kutambua wananchi wangu mnajishughulisha na kilimo ili kujipatia kipato,"alisema.

Mkulima, Christopher Bwagile alisema tangu mwaka 2001 waliomba kibali cha kutumia mto mbarali kwa ajili ya kilimo cha umwagiliji lakini hadi sasa hakuna majibu na ameiomba  serikali ya mkoa huo isimamie upatikanaji wa kibali ili watumie maji kihalali..




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search