Mwanamke achomwa hadi kufa kwa 'kukataa' uchumba...soma habari kamili na matukio360..#share


Na mashirika ya kimataifa
MAAFISA wa polisi katika mji wa kusini mwa India wa Hyderabad wamemkamata mwanamume, Karthika Vanga( 28)  akituhumiwa kumchoma moto mwanamke Sandhya Rani(25)  hadi kufa kutokana na mgogoro wa kimapenzi.



Rani alishambuliwa alipokuwa anaelekea nyumbani  na kwamba alifariki alipokuwa akipelekwa hospitalini.  Mshukiwa Karthika Vanga  ni mfanyikazi mwenzake wa zamani.


Alikuwa akifanya kazi katika kampuni moja na bi Rani hadi miezi michache iliyopita.

Wakati alipomkaribia siku ya Alhamisi wawili hao walionekana wakijibizana kabla ya mwanamume huyo kuchukua mafuta ya taa, na kumwagia mwilini na kumchoma moto , polisi walidai.

Walisema kuwa kulikuwa na madai kwamba Vanga amekuwa akitaka kumchumbia bi Rani kwa kipindi cha miaka miwili.

Alikuwa amekataa mara kadhaa kuchumbiwa na bwana huyo ijapokuwa polisi wanasema haijulikani iwapo kulikuwa na malalamishi dhidi ya mtu huyo.

Mashambulizi dhidi ya wanawake nchini India yameongezeka tangu ubakaji wa gengi la mwaka 2012 na mauaji ya mwanafunzi katika basi moja mjini Delhi, na yamesababisha kuwekwa kwa sheria kali zinazolenga kukabiliana na mashambulio kama hayo.


Tayari nchi hiyo imeshapiga marufuku talaka tatu na wanaume wanaotoa talaka tatu kwa mpigo hufungwa jela  huku  mabibi harusi wanakabidhiwa silaha ya kujilinda India

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search