MO Dewji amtaka Omog aachie ngazi Simba...soma habari kamili na matukio360..#share
Na mwandishi wetu, Dar es
Salaam
KATIKA hali ya sintofahamu
bilionea Mohammed Dewji amemtaka kocha mkuu wa timu ya Simba, Mcameroon Joseph Omog ajiuzulu.
Mohammed Dewji
Bila kutaja sababu Dewji
jioni ya leo majira ya saa kumi Desemba
23/12/2017 katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Facebook ameandika ; "Kwa kuwa bado sina mamlaka ya maamuzi kwenye klabu ya simba, kama
mwanachama na shabiki wa simba, namuomba Omog kwa heshima na taadhima ajiuzulu.’’
Mo ambaye ni mfanyabiashara anatoa kauli hiyo ikiwa ni miezi michache
kushinda dhabuni ya kuwa mwekezaji katika klabu ya Simba.
Mo Dewji alishinda zabuni ya
kuwa mwekezaji wa Simba kwa dau la Sh bilioni 20 alizoweka ‘mezani’ ambapo
Simba sasa inamilikiwa na pande mbili, wanachama na Mohamed Dewji.
Kufuatiwa na kuwa mmilikia
halali wa timu hiyo, Dewji ametoa ahadi kumi kwa klabu hiyo ya Simba.
1. Kambi ya Simba itajengwa
upya kabisa na itakuwa ni hosteli ya kisasa yenye vyumba hadi 35. 30 vitakuwa
kwa ajili ya wachezaji na vitano kwa ajili ya benchi la ufundi.
2.Simba sasa itafaidika kwa
kuwa na gym yake ya kisasa, bwawa kubwa la kuogelea kwa ajili ya mazoezi na
sehemu ya kupumzika kwa wachezaji.
3.Wachezaji, makocha na
viongozi watakuwa na mgahawa wao wa kisasa kabisa.
4. Mo Dewji anaamini timu
lazima iwe na viwanja vya mazoezi. Hivyo ataanza na viwanja viwili, kimoja
nyasi asilia na kingine nyasi bandia.
5. Mo Dewji ameahidi
kuwekeza katika soka la vijana akianza na wale wenye umri wa chini ya miaka 14,
16 na 18 na lengo ni kuwakuza.
6. Mo Dewji amesema atasimamia
wachezaji kuitambua thamani ya Simba kwa kujituma hasa.
7. Simba itaanza kufanya
mambo kimataifa kwa kuitangaza na kuikuza brand ikiwa ni pamoja na kutengeneza
vifaa mbalimbali kama fulana, kofia, vishika ufunguo na kadhalika.
8. Ameahidi kutenga kitita
cha Sh milioni 500 ambazo zitatumiwa na
benchi la ufundi katika mipango yao kama kambi na kadhalika pia Sh bilioni moja
kwa ajili ya usajili.
9. Kushindana na timu kubwa Afrika na sio Tanzania
pekee.
10. Kurejesha Simba katika historia ya kimataifa




No comments:
Post a Comment