Ngono yamfukuzisha kazi naibu waziri mkuu...soma habari kamili na matukio360...#share
Na mashirika ya kimataifa
NAIBU wa waziri mkuu wa
Uingereza, Damian Green, ameachishwa kazi baada ya kubainika kuwa alikiuka
kanuni za uwaziri.
Damian Green
Green ambaye alikuwa
mshirika wa karibu wa Waziri mkuu Theresa May alibainika kuwa alitoa taarifa
zisizo sahihi kuhusu picha za ngono zilizokutwa kwenye kompyuta yake ya
ofisini.
Pia Damian Green alikuwa anachunguzwa juu ya madai ya
kutowaheshimu wanawake wanaharakati katika chama chake cha Conservative.
Hata hivyo kiongozi huyo amekanusha kuhusika na
mashitaka yote yanaomkabili.
Wadadisi wa masuala ya kisiasa wamesema kuondoka kwa
kiongozi huyo ni pigo kubwa kwa waziri mkuu .




No comments:
Post a Comment