Wajue nguruwe wenye sura mbaya zaidi Duniani...soma habari kamili na matukio360..#share

 Na mashirika ya kimataifa
WANASAYANSI  wamepata picha za kwanza za msituni za   nguruwe wachache wenye sura mbaya zaidi duniani.

Mmoja wa nguruwe mwenye sura mbaya zaidi

Nguruwe hao kwa jina Javan waty, wako kwenye hatari ya kuwindwa na kupotea katika makazi yao na wanasayansi wanasema kuwa nguruwe hao tayari wanaelekea kuangamia.

Kamera fiche kwa sasa zimefichua kuwa idadi ndogo ya nguruwe hao bado wanaishi maeneo ya misitu kadha huko Java.

Wanasayansi wanasema kuwa lengo lao ni kulinda makazi ya wanyama hao.
Mkuu wa utafiti huo Dk Johanna Rode-Margono, alisema kuwa wanasayansi walifurahishwa kugundua kuwa nguruwe hao bado wako.

Utafiti wa mwisho kwenye misitu hiyo ulifanywa mwaka 2004 na kuonyesha kuwa idadi ya nguruwe hao ilikuwa ikididimia zaidi.


"Tuliogopa kuwa wote au wengi zaid walikuwa wametoweka."


Kati ya maeneo saba ambayo wanasayansi waliyafanyia uchunguzi wakitumia kamera fiche, ni matatu tu yaligunduliwa kuwa na nguruwe hao.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search