Magufuli: Wajanja walitaka kuchota bilioni 300.....soma habari kamili na matukio360...#share

Na mwandishi wetu, Dar es salaam
RAIS John Magufuli amesema watu wasiokuwa na nia njema walitaka kuchota takriban sh  bilioni 300 kutoka katika mradi wa  mfumo wa uhamiaji mtandao na hati ya kusafiria 'passport' ya kielektroniki.

Rais John Magufuli

Amesema vyombo vya usalama ndivyo vilivyotumika kuokoa wizi huo  na amemtaka kamishna mkuu wa uhamiaji kuongeza mbinu kudhibiti mianya mibovu katika idara hiyo.

Rais Magufuli amesema hayo leo jijini Dar es salaam alipokuwa akizindua mradi huo na  kuwa awali mapendekezo ya mradi huo ilikuwa ni sh bilioni 400 na  hadi unakamilika umetumia sh bilioni 127.2

"Wajanja wachache wasiohitakia mema Tanzania walikuwa wameshatengeneza dili la kuchota zaidi ya mabilioni katika mradi huu, awali walisema ugegharimu sh bilioni 400 lakini kupitia vyomba vya usalama nchini tukagundua kuna wizi unataka kufanyika.

"Tukafuatilia kwa makini tukagundua mchezo huo, tukaudhibiti na sasa umegharimu sh bilioni127.2 tu. Ndio maana hawa wapigaji walikuwa wakipita huku na huku kuweka vipingamizi kuhusu mrdi huu, walifikiri Tanzania bado ni ile ya zamani ya upigaji,’’ amesema   

Rais amesema idara ya uhamiaji ni muhimu kwa usalama na uchumi wa nchini na kwamba bei ya hati mpya ya kusafiria ya kielektroniki itagharimu sh 150,000 kwa miaka kumi ikiwa ni wastani wa sh 15,000 kwa kila mwezi.

Amesema ongezeko la bei ya hati ya kusafiria inatokana na ubora wake na ongezeko la kurasa nyingi kuliko ya zamani  na  imezingatia usalama wa raia na nchi  

Amesema hivi karibuni idara ya uhamiaji  ililega na kuwa uchochoro kwa wahamiaji na wafanyabiashara hasa wafanyabiashara wa dawa za kulevya ikiwamo kupewa  pasipoti mbili kinyume cha sheria na raia wa kigeni kupata kibali cha ukaaji kiholela.

Pamoja na mambo mengine ameahidi kutoa milioni kumi za ujenzi wa ofisi mpya za makao makuu ya idara ya uhamiaji.

Katika hatua nyingine rais Magufuli ameagiza wahamiaji waliongia kinyume cha utaratibu kutafutwa na kukamatwa mahala popote walipo.

"Ninataarifa kuwa kuna wahamiaji 1500 wa kutoka nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wameingia nchini lakini walioripoti ni chini ya 1000 sasa ninaagiza watafutwe mahala popote walipo na hatua za kisheria zichukuliwe,’’ amesema

Amemtaka kamishna wa idara ya uhamiaji, Dk Anna Makakala kuwachukulia hatua za kinidhamu watendaji na watumishi wa idara hiyo wanaokwenda kinyume na utaratibu wa utendaji kazi.

“Jiulize  mhamiaji alifikaje katika mikoa mingine  hivyo wachukulie hatua za kinidhamu wakuu wa uhamiaji wa mikoa waliyopita ikiwamo kuwashusha vyeo,’’ amesema

 Awali Waziri wa mambo ya ndani, Dk Mwigulu Nchemba amesema mradi huo umezingatia mahitaji ya sasa na kwamba wataanza kutoa hati za kusafiria za elekitroniki  kwa Afrika mashariki na vibali vyote kwa njia ya mtandao.


Mradi huo umetengenezwa na kampuni ya HDI grobu ya marekani  kwa  uangalizi wa nchi ya  Ireland

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search