Wanamitindo nchini waunda chama chao....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam
WANAMITINDO nchini wameanzisha chama chao  kinachoitwa FAT, kitachoshughulikia masuala mbalimbali ya wadau hao


Mwanzilishi wa FAT, Mustafa Hassanali akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa chama cha wanamitindo nchini.


Akizungumza na waandishi wa habari  leo jijini Dar es salaam katika uzinduzi wa chama cha wanamitindo Tanzania(FAT), Mustafa Hassanali  amesema lengo la chama ni kuendeleza maslahi ya sekta ya mitindo kwa kuwaunganisha na kugawana ujuzi, uzoefu na rasilimali katika sekta hiyo.

“FAT pia imelenga kukuza na kuimarisha sekta ya mitindo nchini. Sisi kama wabunifu tunaunga mkono juhudi za rais Magufuli katika kuifanya nchi  kuwa katika uchumi wa viwanda vya kati ifikapo 2025 kwa kuongoza katika bidhaa za nguo na vitambaa zinazotoka Tanzania,” amesema Hassanali.

Ameongeza “Sekta ya mitindo Tanzania inakuwa kwa haraka sana, wadau wake wanakumbana na changamoto nyingi lakini bado tuna uhakika wakati wa mafanikio umefika kupitia kuanzishwa kwa chama hiki chenye nia ya kuimarisha uhusiano mzuri wa wafanyaji kazi za mitindo, wadau wa mitindo na nchini na Duniani kwa ujumla.”

Mmoja wa waanzilishi wa chama hicho, Asia Idarous amesema chama hicho kimeundwa kwa ajili ya wadau wote wa sekta ya mitindo na inajumuisha majukwaa mbali mbali kwa ajili ya mitindo, taasisi za mitindo, wanamitindo wa kuonyesha mavazi (models).

Wengine ni wanamitindo wanaopanga muonekano wa mavazi (stylist), wapiga picha wa mtindo, makampuni ya nguo, wazalishaji na wauzaji mavazi na wanaojihusisha na kazi za mitindo na urembo.


Amewahimiza wafanyakazi katika sekta hiyo  kujiunga katika chama ili kupaza sauti zao kwa fursa mpya za mitindo, kutatua changamoto za kazi za mitindo na kupanua mitandao yao.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search