Mkuu idara mipango miji Ilala apoteza fahamu baada kutumbuliwa...soma habari kamili na matukio360....#share

Na mwandishi wetu, Dar es salaam

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda leo amemwagiza mkurugenzi mkoani humo kuwapangia kazi nyingine wakuu wa Idara ya mipango miji manispaa ya Ilala, Paul Mbembela  na wa Ubungo, Hamis Songwe.

Pia Kaimu Mkuu idara ya maendeleo na ustawi wa jamii Ilala, Sapensia Masawe atapangiwa kazi nyingine kwa kushindwa kutekeleza majuku yake

Kufuatia agizo hilo, Paul Mbembela alianguka na kukimbizwa hospitali kwa matibabu. Mkutano huo ulenga kurejesha majibu kwa wakazi wa Dar es salaam waliodhulumiwa mali zao tofauti.


Paul Mbembela aliyevaa shati nyekundu akiwa amesimamishwa leo katika mkutano wa Makonda na wakazi wa Dar es salaam ukumbi wa Diamond Jubilee.
Akipewa huduma ya kwanza

Baadhi ya wakazi wa Dar es salaam waliohudhuria mkutano wa Paul Makonda


Wanasheria waliohudhuria mkutano wa Makonda na wakazi wa Dar es salaam leo

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search