Aliyemtunuku shahada ya uzamivu Grace Mugabe akamatwa Zimbabwe.... soma habari kamili na matukio360....#share

Na mashirika ya kimataifa
NAIBU chansela wa chuo kikuu cha Zimbabwe, Levi Nyagura amekamatwa kuhusiana na utoaji wa wa cheti cha shahada ya uzamivu kwa mke wa rais wa zamani nchini humo Robert Mugabe.
Grace Mugabe
Grace Mugabe alitunukiwa cheti hicho baada ya kusoma kwa miezi michache na hoja yake ikachapishwa mwezi uliopita baada ya kuzuka kwa wito wa kupokonywa shahada hiyo
Tume ya uchaguzi inatarajiwa kumshtaki naibu huyo  kwa utumizi mbaya wa ofisi.
Kile ambacho hakiko wazi ni iwapo bi Mugabe atakamatwa.
Badala ya kusoma miaka kadhaa alipokea shahada yake miezi kadhaa baada ya kusajiliwa katika chuo hicho.
Alikuwa akijaribu kuwa rais wa taifa hilo lakini baada ya jeshi kumuondoa madarakani Robert Mugabe mwezi Novemba mwaka jana harakati zake za kisiasa ziligonga mwamba hatua iliyowafurahisha raia wengi wa Zimbabwe.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search