Makonda: Waliodhulumiwa nyumbani, viwanja warejee Februari 10....soma habari kamili na matukio360...#share



Na mwandishi wetu, Dar es salaam

WANANCHI waliosikilizwa na wanasheria katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Februari 10, 2018  wametakiwa kufika ukumbi wa Diamond Jubilee  kuanzia Saa moja asubuhi ili kupatiwa mrejesho wa malalamiko yao.

Paul Makonda

Mwenasheria wa ofisi ya mkuu wa mkoa huo, Fabiola Mwingira amesema idadi ya wananchi waliojitokeza ni kubwa tofauti na matarajio yao lakini wamejitahidi hadi sasa zaidi ya wananchi 3,000 wamepatiwa huduma..


"Zaidi ya wananchi 3000 wamepatiwa huduma ya msaada wa kisheria ndani ya siku tano kutokana na kudhulumiwa mali zao  lakini kutokana na idadi kuwa kubwa muda wa kusikilizwa umeongezwa hadi kesho," amesema Fabiola



Amesena mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameongeza siku za kusikiliza malalamiko na madai ya waliodhulumiwa ili kuhakikisha wananchi wote waliofika wanasikilizwa na kuhudumiwa.


Hatua hiyo ya Makonda imefikiwa kutokana na idadi kuwa kubwa ya wananchi waliojitokeza kupata msaada wa kisheria.


Taarifa za kuongezwa kwa muda zimepokelewa kwa shangwe na wananchi ambapo wamemsifu Makonda kwa kutanguliza utu mbele kwa kuhakikisha wanyonge wanaipata haki yao waliyotaabika kuitafuta kwa miaka mingi.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search