Mbowe, wenzake wapo polisi kuhojiwa.... soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es salaam

VIONGOZI wakuu sita wa Chadema akiwamo Freeman Mbowe wamefika kituo cha polisi kati jijini Dar es salaam kuitikia wito wa kamanda jeshi la polisi Dar es salaam, Lazaro Mambosasa.

Viongozi wakuu was Chadema wakiinga kituo cha kati cha polisi jijini Dar es salaam

Wengine ni John Mnyika, Halima Mdee, John Mrema, Salum Mwalimu, Ester Matiko, na John Heche.

Hatua hiyo inafuatia wiki iliyopita baadhi ya viongozi hao kufika kituoani hapo na kutakiwa kurejea leo majira ya saa nne asubuhi.

Mkurugenzi wa mawasiliano wa Mambo ya nje, John Mrema amesema kuchelewa kwao, polisi walitaka kwenda kuwakamata.

"Ni mambo ya ajabu polisi walitaka kuja kutukamata kwa sisi kuchelewa tu. Lakini tunakwenda wenye," amesema Mrema

Picha mbalimbali kabla ya viongozi wa Chadema kuingia kituoani kuhojiwa



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search