Mhh! Muhuhubiri asema wanawake ''chanzo cha uovu''.....soma habari kamili na matukio360...#share

Na mashirika ya kimataifa
MUHUBIRI, Nicolas Niyibikora  wa nchini Rwanda huenda akaingia matatani mbele ya vyombo vya sheria baada ya kuwaita wanawake ''chanzo cha uovu''

Muhubiri huyo wa kanisa la Seventh Day Adventist  aliwaambia wanawake kwamba hawapendwi na Mungu wakati wa matangazo ya idhaa ya redio ya Amazing Grace mwezi Januari akionya kuwa ''hakuna lolote jema linaloweza kupatikana kutoka kwa wanawake''.
''Unaposoma Biblia , ni nani aliyeleta dhambi duniani''? Aliuliza na kuongeza, ''sio mwanamume''.
Tayari mahubiri hayo yamewakasirisha wanaharakati huku wale wanaounga mkono usawa wa kijinsia wakiitisha mkutano na vyombo vya habari na kuonya kuwa maneno kama hayo yanaweza kusababisha chuki na mzozo miongoni mwa raia wa Rwanda iwapo hakuna hatua ya haraka itachukuliwa , kulingana na gazeti la Rwanda la New Times.
Kundi la kutetea haki za wanawake liliwasilisha malalamishi yake katika tume ya udhibiti wa vyombo vya habari ambayo inatarajiwa kukutana ili kuzungunmzia kuhusu suala hilo wiki ijayo.
Afisa mkuu, Emmanuel Mugisha aliambia gazeti la New Times kwamba kuna uwezekano idhaa hiyo ikajieleza.
Hata hivyo Kanisa la Seventh Day nchini Rwanda limefanya juhudi za kujitenga na Niyibikora ambaye wanasema alipigwa marufuku kwa miaka ,mitano.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search