Serikali yapata mrahaba bilioni mbili....soma habari kamili na matukio360....#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

SERIKALI imepata mrahaba wa (Final Royalty) wa sh. bilioni 2 sawa na dola za kimarekani 816, 471.52 pamoja na ada ya ukaguzi kiasi cha dola za Marekani 136,078.59.
Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko.

Pia imesema kufuatia merekebisho ya sheria ya madini yaliyofanyika kupitia ‘The written Laws’ (Miscellaneous Amendments) Act, 2017 na kufuatia kusainiwa kwa kanuni za madini za mwaka 2018 na waziri wa madini sasa vibali vya usafirishaji wa madini nje (export permits) ya nchi vitaombwa kwa tume ya madini na kusainiwa na kaimu katibu mtendaji wa tume ya madini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko, amesema mrahaba huo unatokana na mnada wa tatu wa Februari 2 hadi 9, 2018 wa mauzo ya almasi kutoka mgodi wa Mwadui unaomilikiwa na kampuni ya Williumson Diamonds Limited uliofanyika mjinin Antwerp, nchini Ubelgiji.

“Katika mnada huo, jumla ya karati 54,094.47 ziliuzwa kwa thamani ya dola za Marekani 13,607,858.72 sawa na sh.bilioni 30.6 ambapo jumla ya kampuni 145 zilishiriki katika mnada na kuwasilisha zabuni zao za ununuzi na zabuni  1,019 zilizowasilishwa katika mnada huo,” amesema Biteko.

Aidha amesema mrahaba wa awali (Provisional Royalty) uliolipwa kutokana na uthaminishaji wa awali kabla ya mauzo ni dola za Marekani 674,941.78, ada ya Clearance na Inspection dola za Marekani 112,490.30 ambapo jumla yake ni dola za Marekani 787,532.08 sawa n ash. Bilioni 1.7.

Katika hatua nyingine Biteko amesema kuwa ujenzi wa ukuta kwenye mgodi wa Mererani wenye urefu wa kilometa 24.5 upo katika hatua za mwisho kukamilika.

Hivyo kutokana na hatua hiyo kuanzia Februari 19, 2018 mamlka ya vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa kushirikiana na wataalam wa wizara ya madini wataanza zoezi la utoaji wa vitambulisho vya Uraia kwa wananchi wa eneo husika.

Amesema zoezi hilo limelenga kuhakikisha kuwa wananchi watakaoingia katika eneo la usajili na utoaji wa vitambulisho wawe wanatambulika kwa kuwa na vitambulisho vya uraia kwani lengo kuingilia katika eneo hilo la migodi ya Tanzanite litakuwa moja tu. Hivyo, yeyote asiyekuwa na kitambulisho hicho hataruhusiwa kuingia eneo la mgodi.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search