Picha 14: Ona Maafande wa 'Kike' walivyojichanganya PSPF ndani ya Mlimani City kwa 'Mafunzo Maalum'

MAAFISA wa polisi waliokuwa wakishiriki mafunzo ya siku tatu ya polisi Wanawake kutoka Shirikisho la Majeshi ya Polisi Kusini mwa Afrika (SARPCO), wamepata fursa ya kuelewa kwa undani huduma zitolewazo na Mfuko wa Pensheni wa PSPF kupitia mada mbalimbali zilizotolewa na Maafisa wa Mfuko huo katika mafunzo hayo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Katika mafunzo hayo Maafisa hao walikuwa wakiongozwa na Mkuu wa Idara ya Uchunguzi wa Kisayansi, (Forensic Bureau) ya Jeshi la Polisi, Kamishna wa Polisi, (CP), Elice Mapunda, walipata fursa ya kujua uendeshaji wa Mfuko huo ambao wanachama wake ni pamoja na Watumishi wote wa Umma, Sekta binafsi, na watu wote walio katika sekta isiyo rasmi.

Nae Afisa Uendeshaji Mwandamizi wa PSPF, Bi.Amina Mtingwa, aliwaambia maafisa hao wa polisi kuwa, pamoja na kutambua na kusajili wanachama, kukusanya michango na kutunza taarifa za michango ya wanachama na kuweka michango katika vitega uchumi mbalimbali; alitaja majukumbu mengine ya Mfuko kuwa ni pamoja na kulipa mafao kwa wanaostahili kwa mujibu wa sharia, kutunza kumbukumbu za wanachama na wastaafu, kuangalia upya ubora wa mafao, kufanya tathmini ya Mfuko pamoja na kuweka mikakati Imara.

Aidha kwa upande wake, Kaimu Meneja Matekelezo wa PSPF, Bi.Ritha Ngalo, alizungumzia mwongozo wa ujumuishaji wa michango (totalization and period of contribution guidelines 2013) kama ulivyofanyiwa marekebisho kwa polisi waliochangia GEPF na PSPF.

Fuatilia Picha za Matukio mbali mbali wakati mafunzo hayo maalum yalipokuwa yakiendelea – kwa hisani kubwa ya Khalfan Said wa Kv blog.















About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search