SERIKALI:Kila mwezi wanafunzi sekondari wapimwe ujauzito...soma habari kamili na matukio360....#share

Na mwandishi wetu, Mbeya

SERIKALI mkoani Mbeya sasa ameagiza kila mwezi wanafunzi wa kike wa shule za sekondari wapimwe ujauzito.


Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla akizungumza na wanafunzi na wananchi katika Shule ya Sekondari Madibira alipofanya ziara ya kikazi.

Agizo hilo limetokewa na mkuu wa mkoa huo, Amos Makalla katika ziara yake ya
kukagua miundombinu ya vyumba vya madarasa  sita na bweni la wanafunzi
wa kiume katika Shue ya Sekondari Madibira Wilayani  Mbarali

"Sera ya elimu bure, pia  inalenga kuhakikisha mtoto wa kike anapata
elimu  sasa wasimamizi wa wanafunzi katika shule za bweni muwe na
utaratibu wa kuwapima kila mwezi isije kutokea wanasoma wakiwa
na ujauzito," amesema.

Amesema  utaratibu huo ulikuwapo miaka ya nyuma na sasa ameagiza uanze kuanzia leo.

Pamoja na mambo mengine amewataka wanafunzi wa kike kuwapuuza wanaume wanaowalaghai kwa kuwapa pesa na vitu mbalimbali  ili kujenga uhusiano.

"Muwapuuze vijana wanaowalaghai wanawakatisha ndoto zenu za kuwa
mawaziri,wakuu wa mikoa simamieni elimu ndio msingi mkuu wa maisha
yenu na ndio urithi wa baadaye," amesema

Mkuu wa Wilaya  ya Mbarali, Reuben Mfune amesema atasimamia utekelezaji wa agizo
hilo na kuwaagiza wasimamizi wa watoto katika shule za bweni
kutekeleza ili kupunguza mimba za utotoni kwa watoto wa kike.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search