Zaidi ya walimu 800 wahitajika Zanzibar...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwajuma Kombo, Zanzibar

ZAIDI ya walimu 800 wanahitajika katika shule mbali mbali
visiwani Zanzibar ili kupunguza uhaba wa walimu.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amalia  Zanzibar, Riziki Pembe Juma

Hayo yameelezwa na katibu mkuu wa chama cha walimu Zanzibar (ZATU) Mussa Omar Tafurwa katika mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika mwishoni mwa wiki.

Amesema mfumo wa elimu unakabiliwa na changamoto nyingi
ikiwemo upungufu wa walimu, vifaa vya kusomeshea na uhaba wa madarasa.

Amesema hali ni mbaya zaidi kisiwani Pemba na kwa Unguja ni kwa baadhi ya mikoa ya Kaskazini na Kusini.

“Upungufu wa walimu upo kama tulivyosema kisiwani Pemba tu
utafiti utulioufanya ndani ya chama chetu walimu wanaohitajika
ni zaidi ya 800," amesema.

Kuhusu upungufu wa vifaa vya kusomeshea amesema imetokea baada kusitishwa michango.

Hivyo ameomba kutengwa fungu la fedha kwa ajili ya shule ili kukidhi hali halisi ya upungufu huo wa fedha katika shule .

Akizungumzia kuhusu upungufu wa madarasa amesema hali ilivyosasa ni

msongamano mkubwa wa wanafunzi na kwamba darasa linawafunzi kati 70-100. Ingawa hali hiyo imekuwa ikionekana kuwa ni ya kawaida.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search