Balozi wa Sweeden afungua maonesho ya picha...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

BALOZI wa Sweeden nchini Katarina Rangnitt amefungua maonesho ya picha yanayoonesha jinsi wazazi wa kiume wa Tanzania na Uturuki wanavyoshiriki katika malezi ya watoto.


Balozi wa Sweeden nchini, Katarina Rangnitt akizungumza alipokuwa akizindua maonyesho ya picha yanayoonesha jinsi wazazi wa kiume wa Tanzania na Sweeden wanavyoshiriki katika malezi ya mtoto Coco beach jijini Dar es Salaam.

Akizungumza kwenye ufunguzi huo uliofanyika jana Coco beach jijini Dar es Salaam, Rangnitt amesema lengo la maonesho hayo ni kuonesha umuhimu wa wanaume kushiiki katika malezi ya mtoto na kuhamasisha usawa wa kijinsia.

“Ushiriki wa mwanaume kama baba kwenye malezi ya mtoto unaumuhimu mkubwa kwenye maisha ya wanawake, lakini pia unaleta matokeo chanya kwa wanaume wenyewe,” amesema.

Amesema kuwa kwa Sweeden kumepigwa hatua kubwa katika ushiriki kwani wanaume hupewa hata likizo ya uzazi pale wake zao wanapojifungua.

Ameongeza kwamba, baba anapokuwa karibu na familia kabla, wakati na baada ya mtoto kuzaliwa inasaidia kuwa na matokeo chanya katika afya ya mama na mtoto, mama na mtoto hupata msaada wa muda mrefu katika huduma mbalimbali, lakini pia na kuwa na mchango chanya  katika makuzi ya mtoto kiafya na kiakili.

Maonesho hayo ni ya siku sita na kilele chake ni Machi 21, 2018.
Baaadhi ya wazazi walioshiriki katika uzinduzi huo akiwemo msanii wa filamu za kitanzania 'Bongo movie' Singo Mtambalike (wapili kutoka kushoto) wakielezea jinsi wanavyoshiriki katika malezi ya watoto kwenye familia zao.



Baadhi ya watu waliohudhuria kwenye ufunguzi huo




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search