Ushirika watoa tani 120 za saruji ujenzi ofisi walimu.... soma habari kamili na matukio360....#share
Na mwandishi wetu, Dar es salaam
MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amepokea tani 120 za mifuko ya saruji sawa na mifuko 2,400 kutoka kwa vyama vya ushirika 27 vya mkoa huo vilivyoguswa na kampeni ya ujenzi wa ofisi 402 za walimu Dar es salaam.
Ushirika wakimkabidhi tani 120 za saruji mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda
Mifuko hiyo ina uwezo wa kufyatua tofali 70,000 zitakazojenga ofisi 14 za kisasa za walimu.
Akipokea mifuko hiyo jana Makonda amesema shughuli ya ujenzi wa ofisi za walimu inaendelea vizuri na amewashukuru wadau wanaoendelea kuchangia kampeni hiyo inayolenga kuboresha mazingira ya kazi kwa walimu ili waweze kutoa elimu bora kwa wanafunzi.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Ushirika Dar es salaam, Tumaini Wilfred amesema wameguswa na jitiada zinazofanywa na Makonda katika kuboresha mazingira ya walimu na kuwa ni jambojema linalolenga kuleta ukombozi wa fikra.
Tumaini amesema Ushirika utaendelea kuunga mkono kwa kila hali juhudi zinazifanywa na Makonda.
MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amepokea tani 120 za mifuko ya saruji sawa na mifuko 2,400 kutoka kwa vyama vya ushirika 27 vya mkoa huo vilivyoguswa na kampeni ya ujenzi wa ofisi 402 za walimu Dar es salaam.
Ushirika wakimkabidhi tani 120 za saruji mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda
Mifuko hiyo ina uwezo wa kufyatua tofali 70,000 zitakazojenga ofisi 14 za kisasa za walimu.
Akipokea mifuko hiyo jana Makonda amesema shughuli ya ujenzi wa ofisi za walimu inaendelea vizuri na amewashukuru wadau wanaoendelea kuchangia kampeni hiyo inayolenga kuboresha mazingira ya kazi kwa walimu ili waweze kutoa elimu bora kwa wanafunzi.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Ushirika Dar es salaam, Tumaini Wilfred amesema wameguswa na jitiada zinazofanywa na Makonda katika kuboresha mazingira ya walimu na kuwa ni jambojema linalolenga kuleta ukombozi wa fikra.
Tumaini amesema Ushirika utaendelea kuunga mkono kwa kila hali juhudi zinazifanywa na Makonda.
No comments:
Post a Comment