Magufuli: Sitobadilika, aahidi kumega hifadhi kuwapa wananchi....soma habari kamili na matukio360...#share




Na mwandishi wetu, Bukombe
RAIS John Magufuli ameendelea kusisitiza kuwa hatobadilika na ataendelea kuwa yule yule katika kuwatumikia wananchi.

Pia amesema serikali itamega maeneo ya ardhi ya hifadhi na kuwapa wananchi ili yatumike katika shughuli za maendeleo.

Rais John Magufuli

Ametoa msimamo huo leo alipokuwa akifungua matumizi ya barabara ya Uyovu- Bwaga km 45 katika eneo la uyovu runzewe wilayani  Bukombe mkoani Geita.

“Sitobadilika kamwe mimi ni yule yule nitaendelea kuwatumikia watanzania wote,’’ amesema Magufuli

Kuhusu ardhi amesema hatua ya kumega ardhi ya hifadhi ni kufuatia kuwepo kwa ongezeko la idadi ya watanzania tangu  nchi kupata uhuru.

“Ni ukweli usiopingika ni lazima maeneo ya hifadhi yamegwe na kupewa wananchi kwa ajili ya shughuli za maendeleo hii ni kutokana na kwamba idadi ya watanzania imeongeza maradufu tangu nchi ipate  uhuru,’’ amesema Magufuli

Amewata wananchi kuwa na subra na kwamba serikali ipo katika mchakato wa kutoa maeneo hayo.

Rais amesema kutokana na ongezeko la watu maeneo ya kulima na ufugaji yamepungua kwa kiasi kikubwa.

Akitolea mfano amesema kwa sasa matumizi ya ardhi kwa wilaya ya Bukombe ni asilimia 40 na asilimia 60 ni hifadhi.

“Hakuna sababu ya kuandamana wala kupigana kugombea ardhi, serikali itatoa ardhi,’’ alisisitiza.
  
Barabara hiyo ni kiunganishi cha mikoa ya Geita, Shinyanga, Kigoma, Kagera pamoja na nchi ya  Rwanda



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search