Makonda:Wasanii mpo huru Dar es salaam.....soma habari kamili na matukio360...#share
Na mwandishi wetu, Dar es salaam
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametoa kibali cha kuruhusiwa wasanii nchini kurekodi video na filamu eneo lolote wanalotaka ili kutangaza vivutio vya utalii jijini humo.
Pia amepiga marufuku kwa watendaji wanaozuia wasanii kurekodi video za nyimbo au filamu kwenye mandhari (location) mbalimbali za jiji hilo kwa kuwa inalorudisha nyuma utalii.
Waziri wa TAMISEMI, Sulemani Jaffo (kushoto) akizungumza na Paul Makonda
Agizo hilo ametoa jana jijini Dar es salaam katika hafla ya uzinduzi wa kutangaza vivutio vya utalii katika jiji hilo. Mgeni rasmi alikuwa ni waziri wa Tamisemi, Sulemani Jaffo
"Haiwezekani msanii akitaka kurekodi Video au Movie kwenye mitaro ya maji machafu ambayo inatoa taswira mbaya kwa jiji letu hasumbuliwi vibali lakini akirekodi kwenye Hotel, Majengo Marefu, fukwe au kwenye mazingira mazuri anasumbuliwa kibali, hili haliwezekani, kuanzia sasa wasanii mtarekodi Video Location yoyote mnayotaka isipokuwa Ikulu, Mahakama, Maeneo ya jeshi na vituo vya polisi ambapo panahitaji vibali maalumu," alisema Makonda.
Amesema lengo lake mi kuona wasanii wanapewa fursa ya kutangaza vivutio vya utalii kupitia kazi za sanaa wanazokabiliana.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametoa kibali cha kuruhusiwa wasanii nchini kurekodi video na filamu eneo lolote wanalotaka ili kutangaza vivutio vya utalii jijini humo.
Pia amepiga marufuku kwa watendaji wanaozuia wasanii kurekodi video za nyimbo au filamu kwenye mandhari (location) mbalimbali za jiji hilo kwa kuwa inalorudisha nyuma utalii.
Waziri wa TAMISEMI, Sulemani Jaffo (kushoto) akizungumza na Paul Makonda
Agizo hilo ametoa jana jijini Dar es salaam katika hafla ya uzinduzi wa kutangaza vivutio vya utalii katika jiji hilo. Mgeni rasmi alikuwa ni waziri wa Tamisemi, Sulemani Jaffo
"Haiwezekani msanii akitaka kurekodi Video au Movie kwenye mitaro ya maji machafu ambayo inatoa taswira mbaya kwa jiji letu hasumbuliwi vibali lakini akirekodi kwenye Hotel, Majengo Marefu, fukwe au kwenye mazingira mazuri anasumbuliwa kibali, hili haliwezekani, kuanzia sasa wasanii mtarekodi Video Location yoyote mnayotaka isipokuwa Ikulu, Mahakama, Maeneo ya jeshi na vituo vya polisi ambapo panahitaji vibali maalumu," alisema Makonda.
Amesema lengo lake mi kuona wasanii wanapewa fursa ya kutangaza vivutio vya utalii kupitia kazi za sanaa wanazokabiliana.
No comments:
Post a Comment