Man Utd hoi kwa Sevilla.... soma habari kamili na matukio360....#share

Na mashirika ya kimataifa
Manchester United wametupwa nje ya michuano ya ligi ya mabingwa Ulaya hatua ya 16 bora baada ya kuonyesha kiwango kibovu mbele ya Sevilla na kukubali kichapo cha 2-1 Old Trafford.

Wissam Ben Yedder aliyetokea benchi kwa upande wa Sevilla ndiye aliyepeleka kilio kwa Man u baada ya kufunga magoli yote mawili dakika mbili tu baada ya kuingia uwanjani.
Kipindi cha kwanza Man U ilikosa kuongoza baada ya mikwaju ya Marouane Fellaini na Jesse Lingard kuchezwa vyema na mlinda mlango wa Sevilla Sergio Rico aliyeonyesha kiwango bora kwenye mchezo huo.

Romelu Lukaku alifunga kwa upande wa United zikiwa zimesalia dakika saba lakini goli lake halikusaidia kitu.
United inaungana na Tottenham kuyaaga mashindano hayo lakini kinara wa EPL Manchester City na Liverpool tiyari wamefuzu hatua ya robo fainali na sasa wanasubiria kupangwa kwa droo siku ya Ijumaa.
Chelsea wanaweza kuungana nao iwapo wataiondosha Barcelona siku ya Jumatano.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search