Ninje atangazwa kocha Ngorongoro Heroes...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu nchini (TFF), limemtangaza kwa muda, Ammy Ninje, kuwa Kocha wa muda wa Timu ya taifa ya Vijana wenye chini ya miaka 20, Ngorongoro Heroes.

Ninje ametangazwa leo na TFF ilikuiandaa timu hiyo kwa ajili ya  michezo miwili ya kirafiki dhidi ya Morocco na Msumbiji ikiwa ni kabla ya kucheza na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuelekea AFCON U20.

Ngorogoro Heroes itacheza na timu ya Taifa ya Vijana ya Morocco Jumamosi ya Machi 17, 2018 na dhidi ya timu ya Taifa ya Vijana Msumbiji, Jumatano Machi 21, 2018 ambapo michezo hiyo itachezwa katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za AFCON U20, Ngorogoro Heroes itacheza dhidi ya DR Congo Machi 31 katika uwanja wa Taifa, na mchezo wa marudiano utachezwa baada ya wiki mbili jijini Kinshansha Congo.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search